SEKTA YA ELIMU
UWEKAJI JIWE LA MSINGI VYUMBA VITATU (03) VYA MADARASA NA OFISI YA WALIMU SHULE YA MSINGI KANKWALE MANISPAA YA SUMBAWANGA .
Mwenge wa Uhuru ukiwa Katika Wilaya ya Sumbawanga utaweka jiwe la Msingi Ujenzi wa Vyumba vitatu vya Madarasa katika shule ya Msingi Kankwale katika Kata ya Senga Manispaa ya Sumbawanga. Mradi huu umegharimu kiasi cha Tsh 60,952,500 fedha kutoka Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA).
Mradi huu utasaidia kuongeza ubora wa mazingira ya kujifunzia na kufundishia na kuongeza ufaulu kwa Wananfunzi .
SEKTA YA ELIMU
UWEKAJI JIWE LA MSINGI UJENZI WA MADARASA MANNE, CHUMBA CHA WATOTO, VYOO, NA JENGO LA UTAWALA TAASISI YA ELIMU YA WATU WAZIMA MANISPAA YA SUMBAWANGA.
Mwenge wa Uhuru ukiwa Katika Wilaya ya Sumbawanga utaweka jiwe la Msingi Ujenzi wa Vyumba vinne vya Madarasa, Chumba cha Watoto, Vyoo na Jengo la Utawala Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima Kituo kilichopo Nambogo Kata ya Milanzi Manispaa ya Sumbawanga . Mradi huu umegharimu kiasi cha Tsh 320,000,000/= ikiwa ni utekelezahi wa miradi ya SEQUIP.
Mradi huu utasaidia watoto wa kike waliopata changamoto ya kushindwa kuendelea na masomo katika mfumo rasimi, watu wenye mahitaji ya kielimu kuanzia wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu na watu wote wenye uhitaji wa kujiendeleza kielimu kuanzia sekondari hadi elimu ya juu.
SEKTA YA MIUNDO MBINU
UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI KATIKA BARABARA YA TAWAQAL PETROL STATION – HIGH COURT YENYE UREFU WA KM 2.03 ILIYOJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI MANISPAA YA SUMBAWANGA.
Mwenge wa Uhuru ukiwa Katika Wilaya ya Sumbawanga utaweka jiwe la Msingi katika Barabara ya Tawaqal Petrol Sation – High Court katika Kata ya Katandala Manispaa ya Sumbawanga yenye urefu wa Km 2.03 iliyojengwa kwa kiwango cha Lami . Mradi huu umegharimu kiasi cha Tsh 500,000,000/= ikiwa ni fedha za Tozo ya Miamala .
Mradi huu utasaidia kurahisisha shughuli mbali mbali za usafiri na usafirishaji pamoja na kuongeza uboresha wa mji wa Manispaa ya Sumbawanga.
Pia kukamilika kwa barabara hii kumepunguza sana uwezekano wa kuharibika kwa vyombo vya moto hasa Magari, Bajaji na piki piki kutokana na hali halisi ya barabara ilivyokuwa awali.
Sumbawanga Municipal Council
Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga
Simu ya Mezani: +255252802163
Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255
Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz
HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa