JIOGRAFIA YA MANISPAA YA SUMBAWANGA
Manispaa ya Sumbawanga ni Makao Makuu ya Wilaya na Mkoa wa Rukwa ukiwa Kusini Magharibi mwa Tanzania kwenye Latitudo 07045’ na 080 09’ Kusini na Longitudo 310 27’ na 310 49’ Mashariki. Halmashauri hii imezungukwa na Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga, Kalambo na Nkasi.
UKUBWA WA ENEO NA HALI YA KIJIOGRAFIA
Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga ina ukubwa eneo lenye kilometa za mraba 1329.
HALI YA HEWA
Manispaa ya Sumbawanga ina hali ya hewa ya baridi na joto kiasi kwa kipindi kirefu cha mwaka, ikiwa na joto la 270C mwezi Septemba hadi Januari. Hali ya baridi na ukame huanzia mwezi Mei hadi Novemba. Mwezi Julai ni mwezi wa baridi sana ambayo hufikia 50C. Kipindi cha mvua huanza mwezi Novemba hadi Aprili. Wastani wa mvua ni mm 646.8 kwa mwaka mara nyingi huandamana na miungurumo na radi.
IDADI YA WATU KATIKA MANISPAA YA SUMBAWANGA
Matokeo ya Sensa ya mwaka, 2012 yanaonesha kuwa idadi ya watu kwa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga ni 209,793 kati yao wanaume ni 100,734 na wanawake ni 109,059 na kwamba jumla ya watu 62,951 sawa na asilimia 43 wameongezeka kutoka watu 146,842 (Me 71,176 na Ke 75,666) mwaka 2002.Kutokana na wastani wa ongezeko la idadi ya watu la 3.5% mwaka 2016 tunakadilia kuwa na Watu 241,513 kati ya hao Wanaume 115,964 na Wanawake 125,548.
MUUNDO WA KIUTAWALA
Manispaa ya Sumbawanga imegawanywa katika Tarafa mbili za Lwiche na Itwelele, Kata 19, Vijiji 24, Mitaa 167 na Vitongoji 173. Halmashauri ina jimbo moja la uchaguzi ambalo ni Sumbawanga Mjini.
Sumbawanga Municipal Council
Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga
Simu ya Mezani: +255252802163
Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255
Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz
HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa