• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Masuala ya Lishe
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Uratibu na Mipango
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

Wasanii Sumbawanga Waomba Uwekezaji kwenye Utayarishaji wa “Audio” na “Video”

Ilibandikwa: October 13th, 2018

Wasanii wa fani mbalimbali mjini Sumbawanga, Mkoani Rukwa wameeleza kilio chao juu ya utayarishaji mbovu wa sauti za muziki na picha za video unaofanywa na watayarishaji waliopo ndani ya mkoa na kuwaomba wadau wa sanaa kutoka katika mikoa iliyoendelea katika fani hiyo kuja kuwekeza ili waweze kuleta ushindani katika sanaa.

Kilio hicho kimetolewa baada ya Afisa utamaduni wa Manispaa ya Sumbawanga, Charles Kiheka, kuwaita wasanii hao wa fani mbalimbali ili kujua changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo pamoja kuwaelimisha miongozo na taratibu mbalimbali zinazotakiwa kufuatwa ili kutokiuka taratibu za kiserikali katika kufanya shughuli zao za sanaa.

Mmoja wa wasanii wa Hip-hop, Martin Gondwe amesema kuwa ‘studio’ zilizopo zimekosa vifaa vizuri vitakavyomwezesha msanii aliyerekodi nyimbo yake mjini Sumbawanga kuweza kuleta ushindani katika ngazi ya kitaifa na kimataifa.

“Vile vile tukizungumzia upande wa “video”, wasanii wanakuwa wanafanya nyimbo inakuwa na “quality” (ubora) ndogo, “Audio” inakuwa ya kawaida, pamoja na “video” pia inakuwa ya kawaida yaani kila kitu kibovu, huwezi kuifikisha hiyo nyimbo yako sehemu yoyote,” Alisisitiza.

Nae Steven Stanley, msanii wa Hip-hop aliongeza kuwa kutokana na ubovu wa kazi zinazofanywa na watayarishaji wa muziki katika upande wa sauti na picha inapelekea wasanii wengi kushindwa kuwashawishi wadau wa sanaa na hatimae kukosa kusaidiwa ili kuweza kusonga mbele zaidi.

“”Video” zinakuwa ziko “local” kiasi kwamba huwezi ukamshawishi mtu anunue, kwasababu kila mtu anapenda kitu kizuri, kwahiyo mtu akiona “video” nzuri anasema hii nimeipenda na akiona kitu kibaya anasema piga chini, ila ukosefu wa “production” ndio “una-cost” kabisa, kwasababu siwezi nikarekodi nyimbo hapa ambayo “production” ipo “local” halafu nikatuma Dar,” Alibainisha.

Kwa upande wake Charles Kiheka alileza kuwa wasanii hawatakiwi kusubiri sherehe za kiserikali pekee kama fursa ya kujitangaza bali ni jukumu la msanii kuwa mbunifu katika kuandaa matamasha hayo na hatimae kuonana nae ili kuona namna ya kumsaidia katika kukamilisha mipango ya msanii aliyonayo ili kujiongezea kipato kwa kumpa vibali vyote stahiki pamoja na ushauri wa mikataba mbalimbali anayotaka kuingia na wadau wa burudani.

“Leo hii msanii anakwambia serikali iandae “event” aje “kuperform” wasanii wapo wangapi na matukio ya serikali sio ya kila siku, wewe kama mdau wa sanaa, kama msanii ni jukumu lako kuandaa matukio mbalimbali, unakuja na mipango yako ofisini tunaelekezana namna ya kufanya na kuzitafutia ufumbuzi changamoto unazoweza kukabiliana nazo,”Alisema Kiheka.

Katika juhudi za kuhakikisha wasanii hao wanajifunza namna ya kuandaa matamasha, Kiheka anatarajia kuzindua tamasha la “Amka Kijana, Onesha Kipaji Chako” litakalojumuisha mashindano ya sanaa za fani mbalimbali, kuanzia kuimba, kuigiza, ngoma za asili, pamoja na kucheza nyimbo za kisasa (ku-dance) kabla ya kuisha mwaka 2018.

Matangazo

  • TANGAZO LA CHANJO KWA WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO April 26, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2023 March 11, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2023 March 11, 2023
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KAZI ZA UBORESHAJI WA BARABARA KATIKA MANISPAA YA SUMBAWANGA March 01, 2023
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • SHIRIKIANENI NA SERIKALI KULETA MAENDELEO RUKWA-RC MAKONGORO

    March 16, 2025
  • MD PENDO MANGALI-MSIWE MADALALI WA VIWANJA, CHAPENI KAZI

    November 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MANISPAA SUMBAWANGA

    October 01, 2024
  • EDWINE MISASI NAIBU MEYA MPYA MANISPAA YA SUMBAWANGA

    August 27, 2024
  • Angalia zote

Video

MANISPAA YA SUMBAWANGA KUTAFUTA MZABUNI WA KUZOA TAKA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa