• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Masuala ya Lishe
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Uratibu na Mipango
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

UFUNGUZI UJENZI WA STENDI

Ilibandikwa: May 7th, 2019

Manispaa ya Sumbawanga inatarajia kuongeza mapato yake ya ndani kwa zaidi ya Shilingi Bilioni 1 kila mwaka kutokana na uwekezaji utakaofanywa mara baada ya kukamilika kwa ujenzi wa Stendi ya kisasa ya mabasi  inayojengwa kwenye eneo la Katumba Azimio nje kidogo ya mji wa Sumbawanga.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Jacob Mtalitinya katika hafla ya uzinduzi wa ujenzi wa Stendi ya mabasi iliyofanyika Mei 06, 2019 , ikiwa ni moja ya miradi mikubwa kujengwa na Manispaa hiyo.

Mtalitinya alisema mradi huo wa stendi ambao unajengwa na kampuni ya Sumry Enterprises ya mkoani Rukwa unatarajia kugharimu zaidi ya Shilingi Bilioni tano na unatarajiwa kukamilikia mwishoni mwa mwaka huu.

Alisema katika stendi hiyo kunataraji kujengwa sehemu ya maegesho ya mabasi, Daladala, bajaji, bodaboda, Tax zaidi ya 80, vibanda vya kushushia abiria zaidi ya 50, sanjari  vyumba vya maduka 300 ambapo kwa kuanzia kutajengwa  vyumba 10 kwa kuwa mradi huo unatarajiwa kutekelezwa kwa awamu.

Akizungumza kabla kuzindua zoezi hilo la ujenzi Mkuu wa mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo ameipokeza Manispaa ya Sumbawanga hususan Mkurugenzi wake Jacob Mtalitinya kwa ubunifu wa mradi huo ambao utakuwa na fursa kubwa ya kiuchumi na kibiashara kwa wakazi wa Manispaa hiyo.

Mh.Wangabo alisema mradi huo wa stendi ya kisasa unakwenda kufungua eneo jingine la kibiashara katika kijiji cha Katumba na kuzidi kuupanua mji wa Sumbawanga kwani kuna mpango mwingine wa ujenzi wa mji wa kisasa karibu na Stendi hiyo ambapo zaidi ya viwanja 2100 vya makazi, biashara na huduma za kijamii vimepimwa na kuanza kugawiwa wananchi kwaajili ya ujenzi wake.

“Hii Sumbawanga inabadilika, sio Sumbawanga ile ya zamani, nawapongeza sana Manispaa, kwanikupitia stendi hii pia mapato yenu yataongeza kwakuwa katika makadirio ya makusanyo yenu ya mwaka wa fedha 2018/19 mlikadiria kukusanya zaidi ya Bilioni 2.1, sasa hii stendi pekee itawaingiza karibia asilimia 46 ya mapato yenu ya ndani, hongerni sana”.alisema Mkuu huyo wa mkoa.

Kwa upande wao wananchi wa Katumba licha ya kufurahi mradi huo kujengwa kwenye kijiji chao walisema kuwa kijiji chao kimepanda thamani na kuwa mji sasa na kuongeza kuwa tayari wamekwisha ona tija kwenye mradi huo kwani vijana wengi wamepata ajira na akinamama wanafanya biashara ya kuuza bidhaa mbalimba kama vile vyakula.

Matangazo

  • TANGAZO LA CHANJO KWA WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO April 26, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2023 March 11, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2023 March 11, 2023
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KAZI ZA UBORESHAJI WA BARABARA KATIKA MANISPAA YA SUMBAWANGA March 01, 2023
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • SHIRIKIANENI NA SERIKALI KULETA MAENDELEO RUKWA-RC MAKONGORO

    March 16, 2025
  • MD PENDO MANGALI-MSIWE MADALALI WA VIWANJA, CHAPENI KAZI

    November 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MANISPAA SUMBAWANGA

    October 01, 2024
  • EDWINE MISASI NAIBU MEYA MPYA MANISPAA YA SUMBAWANGA

    August 27, 2024
  • Angalia zote

Video

MANISPAA YA SUMBAWANGA KUTAFUTA MZABUNI WA KUZOA TAKA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa