• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Masuala ya Lishe
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Uratibu na Mipango
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

RUKWA BADO HAINA VYOO BORA, WANANCHI WAHIMIZWA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA

Ilibandikwa: September 16th, 2023

Imeelezwa kuwa ni asilimia 34 pekee ya Wakazi wa mkoa wa Rukwa ndio wanaotumia vyoo bora hali ambayo inachangia uwezekano mkubwa wa kupata magonjwa ya mlipuko ikiwapo kipindupindu na Polio kwa watoto.

Akizungumza katika maazimisho ya Siku ya Usafi wa Mazingira Dunia iliyofanyika katika Manispaa ya Sumbawanga Afisa Tawala Msaidizi Donald Nssoko aliyemwakilisha Mkuu wa mkoa wa Rukwa Makongoro Nyerere amesema takwimu hizo za uwepo wa vyoo bora ni chini ya muongozo wa kitaifa ambao unataka mkoa kuwa na angalau wastani wa asilimia 75.

Nssoko amesema takwimu hizo zinatokana na wananchi wengi wanaotumia vyoo licha ya kuwa sio vyoo bora ambavyo havikidhi vigezo vya miongozo ya sekta ya afya.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga Catherine Mashalla alisema program ya kufanya usafi katika Manispaa ni endelevu na kuongeza kuwa mkakati unapangwa ili kumwezesha kila mwananchi kufanya usafi kwenye eneo lake ilihali akiwaomba wananchi kuunga mkono mpango huo.

Naye Katibu Tawala wa wilaya ya Sumbawanga Gabriel Masinga alisema mpango uliopo unakwenda sanjari na kuanzisha mashindano ya usafi kwa wananchi na taasisi za kiserikali na binafsi ili kuchochea tabia ya wananchi kufanya usafi, huku akisikitishwa na vitendo vya baadhi ya wananchi ambao wamekuwa wakila miwa na kutupa ovyo maganda yake barabarani.

Masinga alisema tabia hiyo haileti sifa kwa wakazi wa Sumbawanga, kauli ambayo iliungwa mkono na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Sumbawanga Justine Malisawa aliyewataka wakazi wa mji wa Sumbawanga kuhakikisha mji huo unang’ara kwa usafi kama ilivyo miji mingine inayosifika kwa usafi hapa nchini.


Matangazo

  • TANGAZO LA CHANJO KWA WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO April 26, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2023 March 11, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2023 March 11, 2023
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KAZI ZA UBORESHAJI WA BARABARA KATIKA MANISPAA YA SUMBAWANGA March 01, 2023
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • SHIRIKIANENI NA SERIKALI KULETA MAENDELEO RUKWA-RC MAKONGORO

    March 16, 2025
  • MD PENDO MANGALI-MSIWE MADALALI WA VIWANJA, CHAPENI KAZI

    November 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MANISPAA SUMBAWANGA

    October 01, 2024
  • EDWINE MISASI NAIBU MEYA MPYA MANISPAA YA SUMBAWANGA

    August 27, 2024
  • Angalia zote

Video

MANISPAA YA SUMBAWANGA KUTAFUTA MZABUNI WA KUZOA TAKA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa