• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Masuala ya Lishe
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Uratibu na Mipango
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

RC Wangabo asisitiza usafi katika mahindi kujikinga na Kansa.

Ilibandikwa: February 23rd, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewataka wakulima wote mkoani Rukwa kuhakikisha wanayasafisha mahindi yao kabla ya kuyauza ili kupata soko la uhakika na pia kujiepusha na magonjwa mbalimbali ikiwemo kansa endapo mahindi hayo yatauzwa yakiwa na mchanganyiko wa mahindi yaliyooza na takataka.

Amesema kuwa mahindi yaliyooza yana sumu Kuvu ambayo hutengenezwa yakiwa na upepo na unyevu, sumu ambayo huleta kansa kwenye miili ya binadamu endapo mahindi hayo yatasagwa na athari hiyo haitakuwa kwa watanzania peke yao bali hata walaji waliopo nje ya nchi.

“Muhakikishe kwamba mahindi yale mnayoyachambua hambakishi mahindi yaliyooza na matakataka yale mahindi yaliyooza ni sumu ile inaitwa sumu kuvu inakuja kutengenezwa baadae kukiwa na upepo na unyevu na kusababisha kansa, lakini pia mawe yakiingia kwenye mfumo wa kusaga unga, chakula kikiwa na mawe kitasababisha kidole tumbo, ambapo hadi ufanyiwe upasuaji ndipo upone,” Alisema

Na kuongeza kuwa kwa kufanya hivyo kutasaidia kutangaza bidhaa nzuri zitakazo Mkoa wa Rukwa katika mikoa mbalimbali nchini lakini pia kama usafi huo utazingatiwa utaleta sura nzuri katika soko la kimataifa na hatimae kuitangaza nchi kwa bidhaa zake bora.

Ameyasema hayo alipotembelea kiwanda cha kuzalisha unga cha Mbasira Food Industries kilichopo kata ya Malangali, Wilaya ya Sumbawanga kujionea maendeleo ya kiwanda hicho chenye uwezo wa kuzalisha tani 36,000 za unga kwa mwaka na kuongea na vibarua wa kiwanda hicho waliokuwa wakitenga mahindi mazima na mabovu kwaajili ya uzalishaji.

Nae Mkurugenzi wa Mbasira food Industries Ltd Mikidadi Kassanda amesema kuwa changamoto kubwa wanayopambana nayo katika kununua mahindi kutoka kwa wakulima ni kupata machanganyiko wa mahindi mabovu na kusababisha kupoteza kilo nne za mahindi mabovu katika kila kilo 100 za mahindi wanayouziwa na wakulima.

“Moja ya changamoto tunazokumbana nazo ni ukosefu wa mafunzo bora kwa wakulima juu ya uzalishaji bora wa mahindi na hatimae kupata mahindi yasiyo na viwango,” Alisema.

Matangazo

  • TANGAZO LA CHANJO KWA WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO April 26, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2023 March 11, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2023 March 11, 2023
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KAZI ZA UBORESHAJI WA BARABARA KATIKA MANISPAA YA SUMBAWANGA March 01, 2023
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • SHIRIKIANENI NA SERIKALI KULETA MAENDELEO RUKWA-RC MAKONGORO

    March 16, 2025
  • MD PENDO MANGALI-MSIWE MADALALI WA VIWANJA, CHAPENI KAZI

    November 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MANISPAA SUMBAWANGA

    October 01, 2024
  • EDWINE MISASI NAIBU MEYA MPYA MANISPAA YA SUMBAWANGA

    August 27, 2024
  • Angalia zote

Video

MANISPAA YA SUMBAWANGA KUTAFUTA MZABUNI WA KUZOA TAKA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa