• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Masuala ya Lishe
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Uratibu na Mipango
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

RC Wangabo asisitiza ajira kwa Vijana na kinamama kwa miradi ya ULGSP.

Ilibandikwa: March 19th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amesisitiza wakandarasi wanaoendelea na ujenzi wa barabara zilizochini ya mradi wa uimarishaji miji katika Manispaa ya Sumbawanga kuwapatia vijana ajira ili waweze kufaidika na utekelezaji wa miradi hiyo.

Ameongeza kuwa kwa kufanya hivyo vijana hao watakuwa na ari ya kuitunzana kuilinda miradi hiyo na kufaidi kipato watakachokipata kutokana na kazi mbalimbali watakazokuwa wakizitekeleza amabzo hazihitaji kisomo kikubwa kutekeleza.

“Fedha za miundombinu katika Manispaa yetu ni Bilioni 18, sasa zimewafikia ninyi wananchi kwa shuilingi ngapi? Pamoja na kwamba kuna mitambo hiyo inaendelea lakini kuna kazi ambazo lazima vijana waajiriwe, na sisi tutawasimamia kuhakikisha ya kwamba huu mradi unawanufaisha mnapata ajira, na kina mama pamoja na kwamba kuna kazi hizi za barabara lakini kuna kutayarisha chakula kwa hawa wanaofanya kazi za barabara,” Alisema.

Alisema maneno hayo alipotembelea utekelezaji wa program ya uimarishaji miji (ULGSP) unaosimamiwa na OR – TAMISEMI na kufadhiliwa na Benki ya Dunia kwa zaidi ya shilingi bilioni 23 inayojumuisha miundombinu, mifumo ya utendaji, usimamizi wa masuala ya kimazingira, kuimarisha mifumo ya kifedha na kuboresha upimaji katika mipango ya matumizi bora ya ardhi mijini.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manaipaa ya Sumbawanga Hamid Njovu amesema kuwa kwa ujumla program hiyo itatengeneza Kilometa 11.5 za barabara za lami katika mji wa Sumbawanga kwa kiwango cha “asphalt concrete” na kuahidi kuwa hadi ifikapo mwezi wa tisa mwaka huu miradi hiyo itakuwa imekamilika.

Mmoja wa wananchi waliokuwepo kwenye eneo hilo Barnabas Juakali ametoa shukrani zake kwa serikali ya awamu ya tano kwa kutekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi na kumshukuru Rais Dkt. John Pombe magufuli kwa kutekeleza yale yote aliyoyaahidi.

Matangazo

  • TANGAZO LA CHANJO KWA WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO April 26, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2023 March 11, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2023 March 11, 2023
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KAZI ZA UBORESHAJI WA BARABARA KATIKA MANISPAA YA SUMBAWANGA March 01, 2023
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • SHIRIKIANENI NA SERIKALI KULETA MAENDELEO RUKWA-RC MAKONGORO

    March 16, 2025
  • MD PENDO MANGALI-MSIWE MADALALI WA VIWANJA, CHAPENI KAZI

    November 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MANISPAA SUMBAWANGA

    October 01, 2024
  • EDWINE MISASI NAIBU MEYA MPYA MANISPAA YA SUMBAWANGA

    August 27, 2024
  • Angalia zote

Video

MANISPAA YA SUMBAWANGA KUTAFUTA MZABUNI WA KUZOA TAKA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa