• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Masuala ya Lishe
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Uratibu na Mipango
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

RC Wangabo aishauri Wizara ya Kilimo kujenga vihenge eneo la viwanda la Kanondo.

Ilibandikwa: January 16th, 2019

Katika hali ya kuupendezesha mji wa Sumbawanga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ameishauri wizara ya kilimo nchini kuona namna ya kuhamisha mradi wa ujenzi wa vihenge kutoka katikati ya mji wa Sumbawanga na kuhamishia katika eneo maalum lililotengwa na Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga kwaajili ya ujenzi wa maghala na viwanda ili kuutanua mji na kujenga vihenge hivyo kwa nafasi.

Amesema kuwa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA)tayari wamekwishanunua eneo la ekari 24.6 lenye thamani ya shilingi 298,938,000 lililopo katika eneo maalum lililotengwa kwaajili ya viwanda vidogo, maghala na hotel lililopo Kijiji cha Kanondo, Kata ya Ntendo, Manispaa ya Sumbawanga ambapo mpaka sasa viwanja vilivyouzwa katika eneo hilo ni asilimia 35.

“Sisi tungependa kama mkoa wa Rukwa eneo hili liwekezwe, kwasababu tuna uchumi wa kati wa viwanda, lakini sasa naona bado tunapenda maeneo yet utu, sasa huku nani atakuja aendeleze? Kwakweli huu mradi uje kujengwa huku ntashauriana na wizara ya kilimo..Mh. Waziri..tuone namna ya kuleta huku, kwasababu hapo mnapotaka kujenga ni eneo dogo” Alisema.

Ameyasema hayo alipotembelea eneo hilo maaluma la uwekezaji wa maghala lililililonunuliwa na NFRA miaka miwili iliyopita huku likiwa limeachwa wazi bila ya matumizi yoyote.

Kwa upande wake Kaimu meneja wa NFRA Mkoa wa Rukwa James Marwa alisema kuwa mradi wa vihenge ulianza kabla ya kununuliwa kwa eneo hilo, hivyo ili kuhamisha mradi huo lazima eneo hilo jipya lipimwe upya.

Nae Afisa Mipango miji wa Manispaa ya Sumbawanga Thadeo Maganga amesema kuwa hatachoka kuendelea kuwahamasisha wadau mbalimbali kufika katika eneo hilo ili kuona umuhimu wake na kuweza kuwekeza kwa maslahi ya Manispaa, Mkoa nan chi kwa ujumla.

Ujenzi huo wa Maghala na Vihenge vya kisasa (Silos) utajengwa katika maeneo nane ya kanda saba za wakala ambapo ujenzi huo utaongeza uwezo wa kuhifadhi mahindi kutoka Tani 251,000 za sasa hadi Tani 700,000 ifikapo mwaka 2025.

Mradi huo wa kuongeza uwezo wa kuhifadhi umeanza kujengwa katika Manispaa ya Songea (Ruvuma), Dodoma, Mpanda (Katavi), Makambako (Njombe), Mbozi (Songwe), Sumbawanga (Rukwa), Shinyanga Mjini (Shinyanga), na Babati (Manyara) ambapo Serikali ya Tanzania na Serikali ya Poland zilisaini mkataba wa mkopo wa masharti nafuu Septemba 2015 wa Dola milioni 55 sawa na sh. bilioni 124, kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo, ambao utaongeza uwezo wa hifadhi ya chakula.

Matangazo

  • TANGAZO LA CHANJO KWA WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO April 26, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2023 March 11, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2023 March 11, 2023
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KAZI ZA UBORESHAJI WA BARABARA KATIKA MANISPAA YA SUMBAWANGA March 01, 2023
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • MKURUGENZI PENDO MANGALI AHIMIZA UADILIFU NA UWABIKAJI KWA WAHITIMU RIBM

    June 20, 2025
  • SHIRIKIANENI NA SERIKALI KULETA MAENDELEO RUKWA-RC MAKONGORO

    March 16, 2025
  • MD PENDO MANGALI-MSIWE MADALALI WA VIWANJA, CHAPENI KAZI

    November 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MANISPAA SUMBAWANGA

    October 01, 2024
  • Angalia zote

Video

MANISPAA YA SUMBAWANGA KUTAFUTA MZABUNI WA KUZOA TAKA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa