• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Masuala ya Lishe
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Uratibu na Mipango
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

OFISI YA CAG YAZIDI KUJIPANGA KATIKA UKAGUZI WA KISASA NA WA VIWANGO ZAIDI

Ilibandikwa: September 6th, 2021

Imeandikwa na Sammy Kisika.

Waandishi wa habari na Asasi zisizo za kiserikali Kanda ya Nyanda za Juu Kusini wamesema  mabadiliko ya kiutendaji yanayofanyika kwenye ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali CAG  yanasaidia kuondoa changamoto za hesabu kwenye Taasisi nyingi za serikali na Mashirika ya umma.

Wakizungumza katika Warsha ya Toleo Maalum kwa wananchi na ukusanyaji wa maoni iliyofanyika mwishoni mwa wiki Jijini Mbeya Waandishi hao walisema kuwa kitendo cha Ofisi ya CAG kukusanya Wataalam wa kada mbalimbali kinaondoa changamoto za ukaguzi na hata maelekezo muhimu yatakayoleta tija kwa Idara mbalimbali za serikali.

Waandishi hao wamesema kuwa kulingana na maelezo yaliyotolewa hivi sasa Ofisi ya CAG ina Wataalam wa TEHAMA, Wahandishi, Wachumi, Wabobevyu wa utawala na wengine wengi hivyo inakuwa rahisi kuweza kushauri halmsahauri na hata idara zinginezo katika kutekeleza miradi yao kwa weledi mkubwa.

Akizungumza kwenye Warsha hiyo Mchumi kutoka ofisi ya CAG Emmanuel Philipo alisema kuwa hivi sasa Ofisi ya CAG imekwishaandaa Mpango Mkakati wa miaka mitano kwa kipindi mwaka 2021 hadi 2026 mpango unakwenda kufanya ukaguzi kwa weledi mkubwa zaidi.

Philipo alisema kwenye Mpango huo Ofisi ya CAG itajikita kufanya ukaguzi wa mahesabu kwa kuzingatia Ufanisi (Performance Audit). Ukaguzi wa Kiufundi (Technicla Audit), Ukaguzi wa Kiuchunguzi (Forensic Audit), Ukaguzi Maalum (Special Audit) na ukaguzi wa Mifumo ya TEHAMA (IT Audit).

Mchumi huyo alisema lengo ni kuhakikisha wanafuatilia matumizi ya fedha za serikali na kushauri namna ya utekelezaji kmiradi lakini pia namna ya kutunza kumbukumbu za kifedha ili kuondoa ongezeko la dosari za kiukaguzi na kuzifanya taasisi nyingi kuwa na hati safi.

"Hii leo CAG anauwezo wa kwenda kufanya ukaguzi mradi ukiwa umeanza kutekelezwa au aukiwa unatekelezwa na akatoa ushauri wa kitaalamu iwapo kuna dosasri amezibaini ziwe za kimahesabu au kiufundi hivyo hii inasaidia uwezekano wa wahusika kuingia katika hoja zisizo za lazima, ni mfumo bora na wa kisasi kwa Taifa letu." alisema Philipo

Alisema lengo la Mpango Mkakati huo ni kuwa Ofisi ya CAG iwe ni Taasisi ya kuaminika nay a kisasa kwenye ukaguzi wa Umma na inayotoa huduma za ukaguzi wa viwango vya juu zinazoimarisha Imani kwa umma.

Matangazo

  • TANGAZO LA CHANJO KWA WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO April 26, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2023 March 11, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2023 March 11, 2023
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KAZI ZA UBORESHAJI WA BARABARA KATIKA MANISPAA YA SUMBAWANGA March 01, 2023
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • TANGAZO: KUNYANG'ANYWA VIWANJA VYA WANANCHI WALIOCHUKUA VIWANJA NA KUSHINDWA KUVILIPIA KWA MUDA MREFU

    June 30, 2025
  • MKURUGENZI PENDO MANGALI AHIMIZA UADILIFU NA UWABIKAJI KWA WAHITIMU RIBM

    June 20, 2025
  • SHIRIKIANENI NA SERIKALI KULETA MAENDELEO RUKWA-RC MAKONGORO

    March 16, 2025
  • MD PENDO MANGALI-MSIWE MADALALI WA VIWANJA, CHAPENI KAZI

    November 28, 2024
  • Angalia zote

Video

MANISPAA YA SUMBAWANGA KUTAFUTA MZABUNI WA KUZOA TAKA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa