• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Masuala ya Lishe
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Uratibu na Mipango
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

MWENGE WA UHURU 2022 WAWEKA MAWE YA MSINGI MIRADI MANISPAA SUMBAWANGA

Ilibandikwa: September 21st, 2022


Mwenge wa Uhuru ni Chombo kilichoasisiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mwaka 1961 ikiwa ni tunu na ishara ya kuwepo kwa Taifa huru la Tanganyika. Tangu kuanzishwa kwa mbio hizi, Mwenge wa Uhuru umekua kichocheo kikubwa katika kuimarisha Uhuru wa Nchi, Umoja wa Kitaifa, Kudumisha Amani, kulinda Muungano na kuhamasisha Maendeleo ndani na nje ya Nchi ya yetu.

Mwenge wa Uhuru umekua kichocheo kikubwa kwa Maendeleo katika Halmashauri yetu. Mbio za Mwenge wa Uhuru 2022 katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, utakimbizwa Kilomita 88.8 katika maeneo mbalimbali na utafanya kazi za kuzindua, kukagua, kuweka Mawe ya Msingi na kutoa Mikopo kwa Vikundi. Jumla ya gharama ya Miradi yote ni Shilingi 1,461,109,000

Tunawakaribisha Wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa katika Halmashauri yetu ya Manispaa ya Sumbawanga.

Mwenge wa Uhuru ni Chombo kilichoasisiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mwaka 1961 ikiwa ni tunu na ishara ya kuwepo kwa Taifa huru la Tanganyika. Tangu kuanzishwa kwa mbio hizi, Mwenge wa Uhuru umekua kichocheo kikubwa katika kuimarisha Uhuru wa Nchi, Umoja wa Kitaifa, Kudumisha Amani, kulinda Muungano na kuhamasisha Maendeleo ndani na nje ya Nchi ya yetu.

Mwenge wa Uhuru umekua kichocheo kikubwa kwa Maendeleo katika Halmashauri yetu. Mbio za Mwenge wa Uhuru 2022 katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, utakimbizwa Kilomita 88.8 katika maeneo mbalimbali na utafanya kazi za kuzindua, kukagua, kuweka Mawe ya Msingi na kutoa Mikopo kwa Vikundi. Jumla ya gharama ya Miradi yote ni Shilingi 1,461,109,000

Tunawakaribisha Wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa katika Halmashauri yetu ya Manispaa ya Sumbawanga.

ORODHA YA MIRADI NA GHARAMA ZA UCHANGIAJI KWA MIRADI ITAKAYOTEMBELEWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2022 KATIKA HALMASHAURI YA MANISPAA YA SUMBAWANGA.


NA

JINA LA MRADI

IDARA

MAHALI MRADI ULIPO

SHUGHULI

GHARAMA ZA WACHANGIAJI

1
Mradi wa Vyumba 3 vya Madarasa na Chumba 1 cha Ofisi Shule ya Msingi Kankwale
Elimu Msingi
Kankwale
Kuweka Jiwe la Msingi
HALMASHAURI

WAHISANI

WANANCHI

SERIKALI KUU
JUMLA KUU

9,894,000

 

1,907,000

60,000,000

71,801,000

2
Utoaji wa Mikopo ya 10%
Maendeleo ya Jamii
Mazwi
Kukabidhi mkopo

10,000,000




10,000,000

3
Mradi wa barabara Tawaqal Petrol Station -High Court
TARURA
Katandala
Kuweka Jiwe la Msingi

 

 

 

975,000,000

975,000,000

4
Mradi wa Zahanati Nambogo
Afya
Nambogo
Kukagua

25,000,000


14,308,000

54,000,000

93,308,000

5
Mradi wa Ujenzi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima
Elimu ya Watu Wazima
Nambogo
Kuweka Jiwe la Msingi



315,000,000


JUMLA KUU

44,894,000

             0

16,215,000

1,404,000,000

1,465,109,000




UWEKAJI JIWE LA MSINGI VYUMBA VITATU (03) VYA MADARASA NA OFISI YA WALIMU SHULE YA MSINGI KANKWALE.

 

JINA LA MRADI.

Ujenzi wa vyumba 03 vya madarasa na Ofisi 01 ya Walimu Shule ya Msingi Kankwale.

TAARIFA FUPI YA MRADI

Shule ya msingi kankwale ni miongoni mwa Shule za Msingi zinazomilikiwa na Serikali yenye darasa la Elimu ya awali hadi darasa la saba, Shule ina jumla ya walimu 15 kati yao ME 12 na KE 03 na Wanafunzi 960 kati  yao WAV 458 na WAS 502.

Kutokana na uchakavu wa Miundombinu ya Shule Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) ilitoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 03 vya Madarasa na Ofisi moja ya Walimu.

UTEKELEZAJI WA MRADI.

Mradi ulipata fedha kutoka Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) kiasi cha Tsh. 60,000,000/= (Milioni sitini tu) iliyoingia tarehe 27/12/2021 baada ya mapokezi ya fedha ujenzi ulianza kwa mfumo wa “Force account” hadi sasa ujenzi unendelea.

 

 GHARAMA YA MRADI.

WACHANGIAJI:-    

Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA)    60,000,000

HALMASHAURI:                                   9,894,000

WANANCHI:                                        1,907,000

MATUMIZI:                                            71,801,000

SALIO:                                                            0

TAREHE YA KUANZA MRADI: 21/02/2022

TAREHE YA KUMALIZA MRADI:  21/07/2022

MANUFAA YA MRADI

Kuondoa uchakavu wa vyumba vya Madarasa uliokithiri katika miundombinu ya Shule kwa muda mrefu na kuongeza ubora wa mazingira ya kujifunzia na kufundishia.  Ndugu Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, tunaomba uweke jiwe la Msingi ujenzi wa vyumba 03 vya Madarasa na Ofisi 01 ya Walimu Shule ya Msingi Kankwale.

TAARIFA YA KUKABIDHI MKOPO KWA KIKUNDI CHA VIJANA.

TAARIFA FUPI YA MRADI.
Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga inaendelea kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya 2020/25 kwa kuhakikisha inatoa mikopo kwa vikundi mbalimbali vya Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu ili waweze kujikwamua kiuchumi na kuendesha  maisha kwa ujumla, hii inafanyika kwa kutoa mikopo ya 10% kutoka mapato ya ndani kwa Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu. Lengo kuu ni kuvijengea uwezo wa kujitegemea na kutoa ajira kwa makundi hayo kupitia sekta binafsi.

TAARIFA YA UTEKELEZAJI.
Kwa mwaka wa fedha 2022/23 Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga imetenga kiasi cha shilingi 184,450,900/= kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu. Halmashauri inatoa kiasi cha mkopo wenye thamani Tsh 10,000,000/= kwa kikundi cha Vijana chenye wanachama 5 Mkopo huu ni sehemu ya Mikopo ya Robo ya kwanza ya Mwaka wa Fedha 2022/2023.

GHARAMA:           10,000,000

WACHANGIAJI:-

HALMASHAURI:   10,000,000 


MCHANGANUO WA MKOPO WA: 

Vijana: 10,000,000
TAREHE YA KUANZA MRADI: 21/09/2022
TAREHE YA KUKAMILIKA MRADI: Endelevu

MANUFAA YA MRADI:

  • Kuongeza ajira na ubunifu kwa Vijana
  • Kuongeza kipato cha wanakikundi na Familia zao kwa ujumla,
  • Kuboresha Uchumi wa Wajasiriamali na Kutanua wigo wa ajira kwenye Sekta binafsi.

 

 

UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI KATIKA BARABARA YA TAWAQAL PETROL STATION – HIGH COURT YENYE UREFU WA KM 2.03 ILIYOJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI TARURA MANISPAA YA SUMBAWANGA.

JINA LA MRADI: Ujenzi wa kiwango cha Lami Barabara ya Tawaqal Petrol Station – High Court yenye urefu wa Km 2.03.

TAARIFA FUPI YA MRADI

TARURA Manispaa ya Sumbawanga inajumla ya km 476.34 kati ya kilometa zota, kilometa zilizojengwa kwa kiwano cha Lami ni 31.19, kilometa zilizojengwa kwa kiwango cha Changarawe ni 121.71 na kilometa 324.44 ziko katika hali ya udongo.

Katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali ilitoa fedha kiasi cha Tshs 500,000,000 zilizotokana na Makusanyo ya Tozo na kiasi cha Tshs 500,000,000 kutoka mfuko Mkuu wa Serikali (Jimbo). Fedha hizo zilitumika katika ujenzi wa Barabara yenye urefu wa kilometa 2.03 kwa kiwango cha Lami nyepesi aina ya Double Surface Dressing (DSD).

Kazi zilizofanyika ni kufanya usafi, kukata na kuondoa tabaka la udongo dhaifu, ujenzi wa tabaka la kwanza la changarawe aina ya G7 lenye unene wa mm 200, ujenzi wa tabaka la pili kwa changarawe aina G15 kwa unene wa mm150, ujenzi wa tabaka la tatu kwa changarawe aina G45 kwa unene wa 150mm na ujenzi wa tabaka nne kwa mchanganyiko wa kokoto aina ya CRR kwa unene wa mm150.

Pia barabara hii imemaliziwa juu kwa kutumia kokoto zenye ukubwa wa mm20 na mm10 zilizowekwa na kushindiliwa juu ya Lami.

MAPOKEZI YA FEDHA NA UTEKELEZAJI WA MRADI.

Mradi huu ulitekelezwa kwa awamu mbili tofaouti kwa kutumia mkandarasi mmoja aitwaye M/S SUMRY ENTERPRISE LTD wa Sumbawanga.

 

Awamu ya Kwanza.

Ujenzi wa Km 1.0 Mkataba Na.AE/092/2021-2022/RKW/W/35 kuanzia Barabara kuu hadi Mahakama kuu kwa kutumia chanzo cha fedha kutoka Mfuko Mkuu wa Majimbo.

Mradi huu ulianza tarehe 01/09/2021 na kukamilika tarehe 28/02/2022 kwa gharama ya Tshs 475,000,000.00.

Fedha iliyopokelewa na kulipwa kwa Mkandarasi mpaka sasa ni kiasi cha Tshs 467,271,052.

 

Awamu ya Pili.

Ujenzi wa Km 1.030 Mkataba Na.AE/092/2021-2022/RKW/W/51 kuanzia Mahakama kuu hadi Barabara ya Mwaiseni – Kanisa la Neema kwa kutumia chanzo cha fedha zinazotokana na Makusanyo ya Tozo za Mafuta.

Mradi huu ulianza tarehe 08/11/2021 na kukamilika tarehe 29/04/2022 kwa gharama ya Tshs 499,822,820.00

Fedha zilizopokelewa na kulipwa kwa Mkandarasi ni kiasi cha Tshs 403,099,487.83

MANUFAA YA MRADI

Baada ya kukamilika kwa barabara hii imerahisisha shughuli mbali mbali za usafiri na usafirishaji pamoja na kuongeza kuboresha Mji wa Manispaa ya Sumbawanga. Pia kukamilika kwa barabara hii imepunguza sana uwezekano wa kuharibika kwa vyombo vya moto hasa Magari, Bajaji na piki piki kutokana na hali halisi ya barabara ilivyokuwa awali.

 

TAARIFA YA KLABU YA KUPAMBANA NA UKIMWI, DAWA ZA KULEVYWA, RUSHWA NA ELIMU YA LISHE SHULE YA SEKONDARI KIZWITE 

JINA LA MRADI: Klabu ya kupambana na Ukimwi, Rushwa, Dawa za Kulevywa na Elimu ya Lishe

TAARIFA FUPI YA MRADI

Shule ya sekondari Kizwite ni miongoni mwa shule za sekondari zinazomilikiwa na Serikali yenye kidato cha kwanza mpaka cha sita, Shule ina jumla ya wanafunzi 1764. Aidha, kwa upande wa walimu, shule inajumla ya walimu 53 kwa mchanganuo wa Me 30 na Ke 23.

IDADI YA WANA KLABU: 60

IDADI YA WAWEZESHAJI/WAKUFUNZI WA KLABU: 5

TAREHE YA KUANZA MRADI: 06/11/2011

TAREHE YA KUMALIZA: Endelevu.

MANUFAA YA MRADI: 

Vijana kupata Elimu ya magonjwa ya kujamiiana pamoja na maambukizi ya virusi vya UKIMWI na njia za kujikinga.

Vijana kupata uelewa juu ya athari za unyanyapaa kwa watu waishio na maambukizi ya VVU na UKIMWI mashuleni na katika jamii watokazo.

Kujenga uelewa mzuri unaoridhisha kwa wanafunzi juu ya maswala ya UKIMWI, na Dawa za kulevya.

Kundi la Vijana hususa ni walio mashuleni Kupata elimu juu ya madawa ya kulevya na madhara yake kwao na kwa Taifa zima.

Vijana walio mashuleni kuona umuhimu wa kuwafikia vijana wengine wote katika jamii inayotuzunguka na kujadili juu ya athari za kujiingiza katika matumizi ya dawa za kulevya na athari zake katika Taifa.

Mradi huu umekuwa chachu kwa vijana kujitambua kwa kujua umuhimu wao kwa Taifa hivo kuichukua elimu hii kama endelevu na inayopaswa kurithishwa kidato mpaka kidato na jamii hususa ni katika kundi rika linalotuzunguka.

Vijana kupata mbinu mbalimbali za utoaji taarifa kwa vyombo vya usalama endapo itabainika kuna aina ya uhalifu unaohusiana na utumiaji wa dawa za kulevya katika jamii husika.

 

 KUWEKA JIWE LA MSINGI TAASISI YA ELIMU YA WATU WAZIMA

JINA LA MRADI: UJENZI WA MADARASA MANNE, CHUMBA CHA WATOTO, VYOO, NA JENGO LA UTAWALA.

TAARIFA FUPI YA MRADI:

Mkoa wa Rukwa ni miongoni mwa mikoa mitatu inayotekeleza mradi wa SEQUIP, Mradi huu unahusu ujenzi wa kituo cha mafunzo cha waichana walioshindwa kuendelea na masomo ya sekondari kwenye mfumo rasmi kwa changamoto mbalimbali ikiwemo ujauzito.

UTEKELEZAJI WA MRADI

Mradi huu unatekelezwa kwa “Force  Account”  fedha awamu ya kwanza tarehe 18/02/2022 zilipokelewa  Tsh. 150,000,000/= na fedha awamu ya pili tarehe 16/05/2022 zilipokelewa  Tsh. 170,000,000/= fedha hizi ni kwa ajili ya ujenzi wa madarasa manne ,chumba cha kulala watoto vyoo pamoja na jengo la utawala.

MAKISIO YA MRADI: 320,000,000

MATUMIZI:              302,743,813.51

SALIO:                        17,256,186.49

TAREHE YA KUANZA MRADI: 15/03/2022

TAREHE YA KUMALIZA MRADI: 30/09/2022 

MANUFAA YA MRADI: 

Mradi huu utakapokamilika utatao fursa ya elimu kwa watoto wa kike waliopata changamoto ya kushindwa kuendelea na masomo katika mfumo rasimi, watu wenye mahitaji ya kielimu kuanzaia wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu na watu wote wenye uhitaji wa kujiendeleza kielimu kuanzia sekondari hadi elimu ya juu. 

Maalum za Mwenge wa Uhuru   Kitaifa tunaomba umeweka jiwe la Msingi ujenzi wa vyumba viwili (4) vya madarasa, Chumba cha watoto, vyoo na jengo la Utawala vya Taasis ya Elimu ya Watu Wazima vinavyojengwa kwenye eneo la Nambogo mjini Sumbawanga.  

 

Matangazo

  • TANGAZO LA CHANJO KWA WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO April 26, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2023 March 11, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2023 March 11, 2023
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KAZI ZA UBORESHAJI WA BARABARA KATIKA MANISPAA YA SUMBAWANGA March 01, 2023
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • SHIRIKIANENI NA SERIKALI KULETA MAENDELEO RUKWA-RC MAKONGORO

    March 16, 2025
  • MD PENDO MANGALI-MSIWE MADALALI WA VIWANJA, CHAPENI KAZI

    November 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MANISPAA SUMBAWANGA

    October 01, 2024
  • EDWINE MISASI NAIBU MEYA MPYA MANISPAA YA SUMBAWANGA

    August 27, 2024
  • Angalia zote

Video

MANISPAA YA SUMBAWANGA KUTAFUTA MZABUNI WA KUZOA TAKA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa