• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Masuala ya Lishe
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Uratibu na Mipango
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

MKURUGENZI MTALITINYA ATAKA MIRADI YA AFYA KUWA BORA ZAIDI

Ilibandikwa: February 12th, 2022

Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga Jacob Mtalitinya amewaagiza Watumishi wa sekta ya Afya ya halmashauri hiyo kuhakikisha wanasimamia miradi ya ujenzi wa iliyopo chini yao ili iweze kukamilika kwa ubora kama yalivyo malengo ya serikali.

Agizo la Mkurugenzi huyo limetolewaleo  mara baada ya kukamilika kwa ziara yake ya ukaguzi wa miradi ya ujenzi wa vituo viwili vya afya vya Kata ya Molo na Matanga, zahanati ya Mponda na Nambogo, sanjari na ujenzi wa hospitali ya wilaya inayojengwa eneo la Isofu mjini Sumbawanga.

Mtalitinya alisema halmashauri hiyo imepata uzoefu mkubwa kwenye usimamizi wa miradi ya ujenzi wa madarasa ya fedha za Uviko-19, maarufu kwa jina la ‘Madarasa ya Mama Samia’ambayo ujenzi wake ulisimamiwa na Kikosi kazi cha halmashauri hiyo kikiongozwa na yeye mwenyewe, ambapo miradi hiyo ilikamilika kwa wakati na kuwa na majengo mazuri na bora, hivyo Idara ya Afya yapaswa kuiga mfano huo.

Alisema katika ujenzi wa majengo hayo ya afya yanapaswa kufuatilia kuanzia hatua ya msingi, kuta , paa na hata ukamilishaji wake ili kuondoa uwezekano wa kukutwa na dosari ambazo hazihitaji kuonekana kwenye halmashauri hiyo kwa sasa.

Aidha amemtaka Mganga Mkuu wa halmashauri hiyo kuhakikisha anateua timu yake ndani ya Idara hiyo (CHMT) ambao watagawanywa kwenye makundi kuweza kufuatilia kila kinachofanyika kwenye ,miradi ya afya kila uchwao badala ya kukaa ofisini na kusubiri taarifa kutoka kwa mafundi.

“Mganga Mkuu una kazi nyingi za kufanya na hutaweza kutembelea miradi yote kila siku, sasa yakupaswa kuunda timu ili ije moja kwa moja huku kushirikiana na Kamati za ujenzi ili kuweza kubaini na kurekebisha dosari yoyote inayoweza kujitokeza na kuitafutia ufumbuzi kwa haraka ili miradi yetu iendelee kuwa bora” alisema Mtalitinya.

Katika ziara hiyo ya Mkurugenzi aliyoambatana na timu yake yote ya Wataalamu wa halmashauri hiyo (CMT) alitoa nafasi kwa Wataalamu hao kuweza kutoa ushauri wao kwa kila mradi ili kuhakikisha inajengwa kwa ubora.

Manispaa ya Sumbawanga hivi sasa imepokea fedha kutoka serikalini na inajenga Kituo cha Afya cha Kata ya Molo kwenye kijiji cha Ulinji, kituo cha Afya cha Kata ya Matanga kwenye kijiji cha Kisumba na hospitali ya wilaya ya Manispaa hiyo kwenye eneo la Isofu lilipo kata ya Malangali kando ya barabara iendayo bandari ya Kasanga katika eneo hilo lililopo upande wa kulia katika eneo la makazi mapya.

Matangazo

  • TANGAZO LA CHANJO KWA WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO April 26, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2023 March 11, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2023 March 11, 2023
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KAZI ZA UBORESHAJI WA BARABARA KATIKA MANISPAA YA SUMBAWANGA March 01, 2023
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • SHIRIKIANENI NA SERIKALI KULETA MAENDELEO RUKWA-RC MAKONGORO

    March 16, 2025
  • MD PENDO MANGALI-MSIWE MADALALI WA VIWANJA, CHAPENI KAZI

    November 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MANISPAA SUMBAWANGA

    October 01, 2024
  • EDWINE MISASI NAIBU MEYA MPYA MANISPAA YA SUMBAWANGA

    August 27, 2024
  • Angalia zote

Video

MANISPAA YA SUMBAWANGA KUTAFUTA MZABUNI WA KUZOA TAKA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa