• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Masuala ya Lishe
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Uratibu na Mipango
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

Mkurugenzi Sumbawanga Manispaa Aja na “Talent Search”

Ilibandikwa: March 5th, 2019

Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga Jacob Mtalitinya amewasihi vijana wa Manispaa ya Sumbawanga kujitokeza kwa wingi katika shindano la kutafuta vipaji ili kuitumia fursa hiyo katika kuviibua na kuviendeleza vipaji vyao huku wakiitangaza Manispaa pamoja na Mkoa wa Rukwa kwa ujumla.

Amesema kuwa kwa muda mrefu Mkoa wa Rukwa hasa wilaya ya Sumbawanga imekuwa na sifa ambayo wengi wakiisikia wanakuwa wanatishika hivyo shindano hili ni fursa ya kuonyesha mambo mazuri yanayopatikana ndani ya mji wa Sumbawanga na Mkoa. Ametoa wito kwa wananchi, vijana, pamoja na wazazi kujitokeza na kuwarusu vijana wao kuonyesha vipaji vyao kuvitumia na kuhakikisha wanajiimarisha siku zijazo kujipatia ajira.

“Idara ya maendeleo ya Jamii kwa kushirikiana na Afisa utamaduni tumeona tuwe na hili shindano ambalo litatumika kuibua vipaji lakini pia kuwaendeleza vijana ambao tunaaamini wakiendelezwa watatengeneza ajira, kwahiyo kipaji ni ajira, hivuyo niwasihi sana vijana wa Sumbawanga kutumia nafasi hii kuhakikisha kwamba wanaendeleza vipaji vyao,” Alisisitiza.

Kwa upande wake Afisa Utamaduni wa Manispaa ya Sumbawanga, Kiheka Charles amesema kuwa manispaa ya Sumbawanga ina vipaji vingi na nia ya kuanzisha mashindano hayo ni kutoa muongozo kwa wasanii wenye vipaji mbalimbali kuweza kuyafikia malengo yao.

“Ofisi ya Mkurugenzi kupitia ofisi ya afisa utamaduni Manispaa ya Sumbawanga tuliamua kuandaa shindano hili lenye lengo la kuwasaidia vijana kuitangaza sanaa yao, kukuza vipaji vyao, na kuweza kuitumia sanaa kama chanzo cha ajira na kunufaika, hivyo basi tunaomba wasanii mbalimbali wenye vipaji wajitokeze kwa wingi kushiriki,”Alisema. 

Halikadhalika, baadhi ya wasanii waliohudhuria kwenye mashindano hayo waliupongeza uongozi wa halmashauri kwa kuwathamini na kuwajali na kuomuomba aendelee kuwaibulia vitu vingine ambavyo vitakuwa ni fursa kwa vijana ili kuweza kuitangaza sumbawanga na Mkoa.

Mmoja wa washiriki wa mashindano hayo Switbert Filbert a.k.a Fire Music alisema “Tunamshukuru sana Mkurugenzi kwa kuanzisha shindano kama hili na tunamuomba kama kuna vingine anavifikiria avifanye kwasababu mkoa wa rukwa upo nyuma katika sanaa, michezo na mengine hivyo tunawaahidi watanzania, wanarukwa na Sumbawanga kuwa tutafanya vizuri.”

Aidha, mshiriki mwenzie wa mashindano hayo Daniel Benedicto a.k.a Dabeto alisema “Mashindano haya yakiendelea kwa Mkoa wetu wa Rukwa sana sana Sumbawanga tunaweza tukatoka sana kwasababu wasanii wengi hawapati muda wa kuonyesha vitu vyao wazi kama vile kupata fursa ya “ku-perform” mbele za watu, wengi tulikuwa tunahofu kwamba unaweza kuonyesha sehemu gani, wengi walikuwa wanjificha ndani, hii ni fursa ya kutengeneza mashabiki.”

Mashindano hayo ya “Sumbawanga Talent Search” yenye kauli mbiu “Kipaji ni Zawadi Thamini Sanaa Yako” yanasimamiwa na Afisa utamaduni ambaye pia ni msanii wa “Hip-Hop” aliyedhamiria kushirikiana na Mkurugenzi wa manispaa hiyo kuinua vipaji vya vijana wa Sumbawanga.

Matangazo

  • TANGAZO LA CHANJO KWA WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO April 26, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2023 March 11, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2023 March 11, 2023
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KAZI ZA UBORESHAJI WA BARABARA KATIKA MANISPAA YA SUMBAWANGA March 01, 2023
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • MKURUGENZI PENDO MANGALI AHIMIZA UADILIFU NA UWABIKAJI KWA WAHITIMU RIBM

    June 20, 2025
  • SHIRIKIANENI NA SERIKALI KULETA MAENDELEO RUKWA-RC MAKONGORO

    March 16, 2025
  • MD PENDO MANGALI-MSIWE MADALALI WA VIWANJA, CHAPENI KAZI

    November 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MANISPAA SUMBAWANGA

    October 01, 2024
  • Angalia zote

Video

MANISPAA YA SUMBAWANGA KUTAFUTA MZABUNI WA KUZOA TAKA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa