• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Masuala ya Lishe
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Uratibu na Mipango
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

MAJANGILI 481 WAKAMATWA ZIWA RUKWA, NYAVU ZAO ZATEKETEZWA

Ilibandikwa: November 8th, 2021

Imeendikwa na Sammy Kisika.

Jumla ya Majangili 481 waliokutwa na zana haramu wakizitumia kwaajili ya kuvua samaki kwenye Ziwa Rukwa wamekamatwa na kutaifishwa kwa mali zao zikiwapo nyavu haramu zenye thamani ya zaidi ya Shilingi Milioni 170 ambazo zimeteketezwa kwa moto.

Kukamatwa kwa watu hao kunafuatia misako ndani Ziwa hilo kwa kipindi cha takribani mwaka mmoja ambapo Majangili hao wametiwa mikononi na Kikosi cha doria cha Pori la Akiba la Uwanda ambao wamefanikiwa pia kuwapiga faini la ya Shilingi Milioni 246.1 ambayo iliwahusisha wavuvi hao sanjari wafugaji waliokuwa wakichungia na kunywesha maji mifugo maeneo ya hifadhi ya Ziwa hilo.

Meneja wa Pori hilo la Akiba la Uwanda Orest Njau amesema kumekuwa na mikakati endelevu ya kudhibiti wavuvi kwenye Ziwa hilo na kuongeza kuwa katika kipindi hicho jumla ya Injini 25 za boti na maboti 19 yalikamatwa yakiwa yanavua kinyume cha taratibu ya maeneo ya hifadhi hiyo.

Njau alizitaja zana zingine zilizokamatwa ni pamoja na ngalawa 90, mitumbwi 72, baiskeli 31, mikokoteni miwili na matanki ya mafuta 17.

Alisema kikosi hicho kimekuwa kikifanya doria za ndani na nje ya Ziwa ili kukabiliana na vitendo hivyo vya uvuvi haramu ili kukabiliana na wavuvi wasiotii sheria kwenye kambi za Mahameni, Mchangani, Mashwiche iliyopo wilayani na mkoa wa  Songwe.

Akizungumza katika zoezi la kuteketeza nyavu 141 za wavuvi hao, Mkuu wa wilaya ya Sumbawanga Sebastian Waryuba alisema kuwa iko haja ya wananchi wa vijiji jirani kuwakumbusha wavuvi wanaovua kwenye Ziwa hilo historia ya muda mrefu ya Ziwa hilo.

Waryuba alisema kuwa iwapo vitendo hivyo haramu vikiendelea samaki ndani ya Ziwa hilo watatoweka na litabaki tupu huku wavuvi waliopo watandoka huku uchumi wa wakazi wa maeneo hayo ya Ziwa Rukwa ukizidi kuporomoka hivyo hawana budi kupinga vitendo vya uvuvi haramu.

Hatahivyo Mkuu huyo wa wilaya ameiomba serikali kupitia Wizara husika kupambana na kutoa maelekezo kwa viwanda vinavyozalisha nyavu hizo haramu kuacha kufanya hivyo badala ya mapambano na wavuvi pekee.

Ziwa Rukwa ni Ziwa linatoa kitoweo cha samaki aina ya Magege na Kambale wanaopendwa sana ndani na nchi jirani kama Jamhuri ya Kidemkokrasia ya Congo, achilia mbali wakazi wa Manispaa ya Sumbawanga ambao ni walaji wakubwa wa samaki hao.

Matangazo

  • TANGAZO LA CHANJO KWA WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO April 26, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2023 March 11, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2023 March 11, 2023
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KAZI ZA UBORESHAJI WA BARABARA KATIKA MANISPAA YA SUMBAWANGA March 01, 2023
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • SHIRIKIANENI NA SERIKALI KULETA MAENDELEO RUKWA-RC MAKONGORO

    March 16, 2025
  • MD PENDO MANGALI-MSIWE MADALALI WA VIWANJA, CHAPENI KAZI

    November 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MANISPAA SUMBAWANGA

    October 01, 2024
  • EDWINE MISASI NAIBU MEYA MPYA MANISPAA YA SUMBAWANGA

    August 27, 2024
  • Angalia zote

Video

MANISPAA YA SUMBAWANGA KUTAFUTA MZABUNI WA KUZOA TAKA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa