• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Masuala ya Lishe
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Uratibu na Mipango
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

KUKAMILIKA KWA UJENZI VYA VITUO VYA AFYA KWAONGEZA UHABA WA WATUMISHI H/MANISPAA YA SUMBAWANGA

Ilibandikwa: April 11th, 2022

Anaandika Sammy Kisika.

Halmasahauri ya Manispaa ya Sumbawanga imepeleka maombi maalumu serikali ya kuomba kuajiri watumishi wa idara ya afya zaidi ya 200, ili kuweza kutoa huduma kwenye zahanati, vituo vya afya na hospitali ya wilaya.

Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo Sebastian Siwale amesema mahitaji ya watumishi hao yanatokana na fedha nyingi zilizotolewa na serikali kwaajili zahanati nne zilizokamilishwa ujenzi wake, huku vituo vya Afya viwili vikajengwa kwenye kata zilizopo nje ya mji na hospitali ya wilaya ya Manispaa hiyo iliyojengwa eneo la Isofu.

Dk. Siwale alizitaja zahanati zilikouwa zimejengwa kufikia hatua ya mamboma kisha serikali ikatoa fedha za kumaliziwa ni pamoja na ile ya kijiji cha Kankwale, Mponda, Nambogo na Fyengeleza.

Wakati vituo vya Afya vinavyoendelea kujengwa ni kile cha Kata ya Mollo na Matanga ambapo vyote kwa pamoja serikali imetoa takribani shiilingi Bilioni moja kujenga vituo hivyo.

Mganga huyo amesema serikali inaendelea kuiboresha sekta ya afya katika Manispaa hiyo ambapo fedha nyingi zimetolewa kwa kiasi cha Shilingi Bilioni 1.5 kukamilisha ujenzi wa hospitali ya  wilaya ya Isofu na nyongeza ya Shilingi Milioni 300 kwaajili kuanza kununua vifaa tiba ili huduma zianze kutolewa wakati wakisubiri fedha za ujenzi wa wodi za wajawazito na watoto katika hospitali hiyo.

Alisema kupatika na kwa fedha hizo ni hatua kubwa ya mafanikio kwa halmashauri hiyo ambayo huduma za afya zinazidi kuboreshwa tofauti na siku za nyuma.

“Kwa kweli tunampongeza sana Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan, kwasababu hivi sasa maeneo mengi ya pembeni ya mji yanasogezewa huduma za afya kwa maana ya ujenzi wa zahanati na vituo vya afya, tunamshukuru sana”.alisema Dk.Siwale

Hatahivyo alisema tayari serikali imetoa fedha kwaajili ya vituo vya afya katika kata ya Senga, achilia mbali kituo cha afya cha kata ya Sumbawanga ambacho kitajengwa na fedha za makusanyoi ya ndani za halmashauro hiyo.

Dk.Siwale alisema kuwa ongezeko hilo la vituo vya kutolea huduma ndilo linaongeza mahitaji ya watumishi wa Idara hiyo ikiwa ni pamoja na Madaktari, Wauguzi, Mafundi sanifu wa maabara, pamoja maeneo mengine mengi.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga Jacob Mtalitinya ,ujenzi wa hospitali ya wilaya ya halmashauri hiyo eneo la  Isofu utakwenda sanjari na unjenzi wa barabara ya lami ya kilometa mbili kwenye barabara ya kuingia na kuzunguka eneo hilo la hospitali ili kurahisisha utoaji wa huduma pamoja kujenga unadhifu wa maeneo hayo.

Mtalitinya ambaye naye hakuishiwa shukrani kwa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendele kutoa fedha za ujenzi hospitali hiyo ambayo ni muhimu kwa wakazi wa mji wa Sumbawanga kwakuwa  itapunguza msongamano katika hospitali tegemezi kwa sasa ya hospitali ya  Rufaa ya mkoa wa Rukwa.

Mtalitinya alisema ili kuendelea kuboresha huduma katika hospitali hiyo ya Isofu, halmashauri imeingia mkataba na Shirika la Nyumba kwaajili ya ujenzi wa nyumba za kisasa kwenye eneo hilo, lakini pia maeneo ya huduma zingine kama vile viwanja vya michezo vya kisasa vitajengwa maeneo ya pembeni ya hospitali hiyo.

Kwa upande wake Mbunge wa Sumbawanga mjini Aesh Hilaly alisema huduma za afya katika halmashauri hiyo zinaendelea kuboreshwa kulingana na jiografia ya maeneo husika ili kuzidi kuzisogeza karibu.

Aesh alisema katika mwaka huu wa fedha wanatarajia kupata fedha kwaajili ya kukamilisha ujenzi wa zahanati za kijiji cha Milanzi na kujenga zahanati na Kinamwanga ambazo zimeanza kujengwa zikiwa kwenye hatua za awali.

Matangazo

  • TANGAZO LA CHANJO KWA WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO April 26, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2023 March 11, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2023 March 11, 2023
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KAZI ZA UBORESHAJI WA BARABARA KATIKA MANISPAA YA SUMBAWANGA March 01, 2023
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • SHIRIKIANENI NA SERIKALI KULETA MAENDELEO RUKWA-RC MAKONGORO

    March 16, 2025
  • MD PENDO MANGALI-MSIWE MADALALI WA VIWANJA, CHAPENI KAZI

    November 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MANISPAA SUMBAWANGA

    October 01, 2024
  • EDWINE MISASI NAIBU MEYA MPYA MANISPAA YA SUMBAWANGA

    August 27, 2024
  • Angalia zote

Video

MANISPAA YA SUMBAWANGA KUTAFUTA MZABUNI WA KUZOA TAKA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa