• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Masuala ya Lishe
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Uratibu na Mipango
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

HAKUNA MCHEZO KWA WATAKAOVURUGA MIRADI YA UVIKO-19 -MTALITINYA

Ilibandikwa: November 17th, 2021

Anaandika Sammy Kisika.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga Jacob Mtalitinya amewatahadharisha wasimamizi  wa miradi ambayo inajengwa kwa fedha zilizotolewa na Rais Samia Suluhu za ufadhili wa  Uviko-19 kuhakikisha zinafanya kazi kulingana na malengo huku akiahidi kupambana na wote watakaokiuka maagizo ya Kamati ya ujenzi.

Manispaa hiyo imepokea kiasi cha Shilingi Milioni 980 kwaajili ya ujenzi wa madarasa 49 ya shule za Msingi na sekondari.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa miradi hiyo ambayo ameitembelea na kutoa ushauri kwa Wasimamizi hao kwa muda wa siku tatu, Mtalitinya alisema kuwa anaamini Wakuu wa shule hizo watafuata yale waliyoelekezwa ili kuweza kukidhi vigezo vilivyotolewa na ofisi ya TAMISEMI kuhusu ujenzi huo.

Mkurugenzi huyo alisema kuwa asingelipenda kuona halmashauri yake inaingia kwenye doa la kuwa chini ya kiwango kwa ujenzi wa  vyumba hivyo vya madarasa hivyo ameamua kuweka mikakati kwa kuanza kutoa semina ya namna ya ujenzi wa miradi hiyo lakini pia yeye mwenyewe kupita kwenye maeneo yote ya ujenzi akiwa na Wataalamu ili kutoa ushauri wa kiufundi na mazingira.

Hatahivyo katika ukaguzi huo Mkurugenzi ametumia muda mwingi kukagua ubora wa madarasa hayo sanjari na maelekezo mengine ya matumizi ya kibajeti ili kuweza kuzitumia fedha hizo kwa usahihi.

“Haya majengo yajengwe vizuri na kwa ubora lakini pia yakamilike kwa wakati na jitihada za makusudi ziwekwe kuhakikisha ununuzi wa viti vya wanafunzi ili watakaoanza masomo kwa kidato cha Kwanza mwakani wasipate shida”.alisema Mtalitinya.

Aidha kwenye ukaguzi huo Mtalitinya ameoneka akitembea na Mkanda wa vipimo “Tape” kwaajili kuhakiki vipimo vyote vya ujenzi wa majengo hayo huku akikosoa pale ambapo vipimo na michoro imekiukwa au kukosewa.

Pamoja na ukaguzi huo Mkurugenzi huyo alisema utaratibu wa ujenzi wa miradi ya Uviko-19 umeonekana kuwa ni mzuri hivyo timu yake ya Wataalamu (CMT) imependekeza kuwa ni utaratibu wa kudumu ambao utatumiwa kwenye miradi ijayo ya halmashauri hiyo.

Katika utaribu huo mpya Wakuu wa Shule wanatakiwa kuwa kwenye eneo la mradi wakiwa na nyaraka zote za mradi, dodoso la maagizo waliyoyapata kwa Wataalamu na Mkurugenzi, sanjari na kupitia hesabu kila siku juu ya kile kilichoagizwa ili kuondoa uwezekano wa kufanya mambo mengine kinyume na mikataba ya miradi hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA CHANJO KWA WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO April 26, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2023 March 11, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2023 March 11, 2023
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KAZI ZA UBORESHAJI WA BARABARA KATIKA MANISPAA YA SUMBAWANGA March 01, 2023
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • SHIRIKIANENI NA SERIKALI KULETA MAENDELEO RUKWA-RC MAKONGORO

    March 16, 2025
  • MD PENDO MANGALI-MSIWE MADALALI WA VIWANJA, CHAPENI KAZI

    November 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MANISPAA SUMBAWANGA

    October 01, 2024
  • EDWINE MISASI NAIBU MEYA MPYA MANISPAA YA SUMBAWANGA

    August 27, 2024
  • Angalia zote

Video

MANISPAA YA SUMBAWANGA KUTAFUTA MZABUNI WA KUZOA TAKA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa