• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Masuala ya Lishe
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Uratibu na Mipango
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

DC Nkasi asisitiza kufikishwa elimu ya UKIMWI kwenye vitongoji.

Ilibandikwa: December 1st, 2017

Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mh. Said Mtanda ameisisitiza idara ya maendeleo ya jamii wanaoshughulikia usambazaji wa elimu ya Ukimwi katika Mkoa na Halmashauri kuhakikisha elimu ya UKIMWI inawafikia watu wa makundi yote hadi katika ngazi ya vitongoji.

Amesema kuwa wananchi wa vijijini ndio wenye kuihitajia zaidi elimu hiyo kuliko wa mjini ambapo kuna utitiri wa vyombo vya habari na ofisi nyingi zinazoshughulika na kutoa huduma hiyo kuliko vijijini ambapo upatikanaji wa taarifa na elimu hiyo ni changamoto.

“Niataendelea kuwasisitiza watu wa maendeleo ya jamii wakishirikiana na masirika mbalimbali yanayotoa elimu ya UKIMWI kuhakikisha kuwa wanawafikia wananchi wa vijijini, kwani hadi hii leo kuna watu huko vijijini hawajui matumizi ya kondomu na matokeo yake kondomu hiyo moja inatumika zaidi ya mara mbili, mtu anifua na kuitumia tena,” Mh. Mtanda alisisitiza

Ameyasema hayo katika maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani yaliyofanyika Kimkoa katika Viwanja vya shule ya Msingi Ndua, Kizwite, Manispaa ya Sumbawanga aliyemuwakilisha mgeni rasmi wa maadhimisho hayo Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo.

Aidha amewatahadharisha wananchi kuwa kupata UKIMWI haina maana kuwa ni marehemu mtarajiwa bali yeyote atakayeupata ugonjwa huo azingatie ushauri wa wataalamu na kufuata masharti ili aweze kuendelea kuishi na kusaidia kujenga taifa letu.

Kwa upande wake Deo Crispin Mlori aliyeishi na UKIMWI kwa miaka 27 amesema kuwa kwa kufuata masharti wamekuwa wakiishi vizuri yeye na mke wake ambao hadi hivi sasa wana watoto wanne wanaowasomesha kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu.

Awali akisoma risala afisa maendeleo ya jamii Mkoa Aziza Kaliatila amesema kuwa kiwango cha maambukizi kwa mkoa wa Rukwa ni asilimia 6.2, kiwango ambacho kipo juu ya maambukizi ya UKIMWI kitaifa.

“Jumla ya wananchi 308727 wamejitokeza kupima VVU ikiwa wanawake 167623 na wanaume 141104 kwa mwaka2016/2017. Waliokutwa na maambukizi ni 4620 Wanawake 2602 Wanaume 2018.” Aziza alifafanua.

Ameongeza kuwa Mkoa umekuwa ukifanya uhamasishaji wa mapambano dhidi ya UKIMWI kwa kutumia gari la sinema Jumla ya vijiji 89 na Kata 36 zimefikiwa kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

“Mkoa pia umeendelea kutoa misaada ya kibinadamu kwa vikundi WAVIU vya 34 kwa gharama ya Shilingi 43,000,000 na watoto yatima wapatao 611 wamelipiwa  ada za shule jumla ya Shilingi 24,070,000.” Amesema.

Matangazo

  • TANGAZO LA CHANJO KWA WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO April 26, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2023 March 11, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2023 March 11, 2023
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KAZI ZA UBORESHAJI WA BARABARA KATIKA MANISPAA YA SUMBAWANGA March 01, 2023
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • SHIRIKIANENI NA SERIKALI KULETA MAENDELEO RUKWA-RC MAKONGORO

    March 16, 2025
  • MD PENDO MANGALI-MSIWE MADALALI WA VIWANJA, CHAPENI KAZI

    November 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MANISPAA SUMBAWANGA

    October 01, 2024
  • EDWINE MISASI NAIBU MEYA MPYA MANISPAA YA SUMBAWANGA

    August 27, 2024
  • Angalia zote

Video

MANISPAA YA SUMBAWANGA KUTAFUTA MZABUNI WA KUZOA TAKA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa