• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Masuala ya Lishe
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Uratibu na Mipango
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

ALAT Rukwa waishauri Wizara ya Maji kutumia wataalamu wa halmashauri kusanifu miradi ya maji.

Ilibandikwa: May 21st, 2018

Wajumbe wa mkutano wa ALAT mkoa wa Rukwa wameishauri Wizara ya Maji kutuwatumia wataalamu wa Halmashauri husika katika kusanifu miradi ya maji kwenye halmashauri zao ili kuondoa uwezekano wa miradi mingi kushindwa kufanikiwa katika utekelezaji wake.

Akizungumza katika kikao kilichofanyika mjini Matai wilayani Kalambo, Mwenyekiti wa ALAT mkoa wa Rukwa Mh.Kalolo Ntila alisema kuwa hoja nyingi zinazotokea katika miradi ya maji zimekuwa zikichangiwa na sababu nyingi na moja wapo ikiwa ni usanifu wa miradi ya maji unaofanywa na Wataalamu toka nje ya halmashauri zao usiozingatia hali halisi ya mazingira na vigezo vya maeneo husika .

Mh.Ntila alisema kumekuwa na changamoto nyingi zinazotokea katika utekelezaji wa miradi hiyo baada ya ujenzi wake maji kushindwa kuwafikia wananchi au kufika kwa kiwango cha chini kutokana aidha mradi kujengwa kwenye vyanzo vya maji visivyo na uhakika au sababu zinginezo za kimazingira.

“Wataalamu wa halmashauri na wananchi wa maeneo yetu wanayafahamu vyema mazingira yao, hivyo ipo haja ya wataalamu wanaotoka nje ya halmashauri kuwashirikisha kabla ya mradi kuanza kujengwa ili nao watoe ushauri wao na kuepukana na changamoto zinazoweza kutokea hapo baadaye”.alisema Ntila

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Manispaa ya Sumbawanga Mh.Jastin Malisawa alisema kuwa Wataalamu wa maji wa halmashauri wana weledi wa kutosha katika utendaji wa kazi zao kama walivyo wale kutoka Wizara ya maji hivyo hakuna sababu ya kuwatenga katika usanifu wa miradi ya maji kwakuwa hata vyuo walivyosoma ni vya aina moja.

Mh.Mwanisawa alisema Wataalamu wote ni watumishi wa serikali hivyo ingelipendeza iwapo kila mtu akashiriki katika kutoa ushauri wake ili Taifa liweze kupiga hatua kubwa ya maendeleo na kwa kasi zaidi pasipo kupata vikwazo vya miradi yake kutekelezwa katika kiwango kisichoridhisha, hali inayochangia kuongeza kwa fedha katika kubadili mifumo ya usanifu wa miradi hiyo au gharama za nyongeza za kuwalipa wakandarasi.

Katika tathimini ya kikao hicho kuhusu miradi ya maji Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga ilionekana kufanya vizuri zaidi, ikifuatiwa na halmashauri ya wilaya ya Kalambo, wakati halmashauri ya wilaya ya Nkasi ikionekana kuwa na changamoto nyingi katika miradi yake.

Matangazo

  • TANGAZO LA CHANJO KWA WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO April 26, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2023 March 11, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2023 March 11, 2023
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KAZI ZA UBORESHAJI WA BARABARA KATIKA MANISPAA YA SUMBAWANGA March 01, 2023
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • SHIRIKIANENI NA SERIKALI KULETA MAENDELEO RUKWA-RC MAKONGORO

    March 16, 2025
  • MD PENDO MANGALI-MSIWE MADALALI WA VIWANJA, CHAPENI KAZI

    November 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MANISPAA SUMBAWANGA

    October 01, 2024
  • EDWINE MISASI NAIBU MEYA MPYA MANISPAA YA SUMBAWANGA

    August 27, 2024
  • Angalia zote

Video

MANISPAA YA SUMBAWANGA KUTAFUTA MZABUNI WA KUZOA TAKA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa