• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Masuala ya Lishe
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Uratibu na Mipango
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

AHADI ZA UJENZI WA UWANJA WA NDEGE SUMBAWANGA WAWACHOSHA WANANCHI

Ilibandikwa: October 6th, 2021

Anaandika Sammy Kisika.

Wajumbe wa Kikao cha Bodi ya Barabara ya mkoa wa Rukwa wameoneshwa kuhuzunishwa kwao na namna Wizara ya Ujenzi inavyochelewesha kuanza kwa shughuli ya ujenzi kwa kiwango cha lami kwa uwanja wa ndege wa Sumbawanga ambao kwa muda mrefu umekuwa ukitajwa kuwa utajengwa.

Mwenyekiti wa kikao cha Road Board ambaye pia ni Mkuu wa mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti amesema hali inaonesha kuwa wananchi mkoani Rukwa wamechoshwa na ahadi za mara kwa mara kuhusu ujenzi wa uwanja huo ambao tayari wananchi waliokuwa pembezoni mwa uwanja wamekwishalipwa fidia takribani miaka mitatu iliyopita.

Mkirikiti amesema pamoja na kuwalipa fidia wananchi hao lakini pia Mkandarasi wa kujenga uwanja huo alishapatikana  ambaye ni M/S Sino-Shine Overseas Construction & Investment East Africa Ltd kwa thamani ya Shilingi Bilioni 55.

Amesema kucheleweshwa kwa ujenzi wa uwanja huo kumekuwa kukileta adha kubwa kwa wasafiri na huduma za ndege kwa mkoa wa Rukwa ambapo wananchi wanalazimika kwenda kupanda ndege mikoa jirani ya Songwe na Katavi.

“Ufike muda sasa tuachane na maneno, wananchi waambiwe ukweli kuwa ni lini kazi hii inaanza lakini siku zote wamekuwa wakipewa ahadi ya siku za karibuni kazi itaanza na hakuna kinachofanyika”.aliema Mkirikiti akiungwa mkono na wajumbe wa kikao hicho.

Uwanja wa ndege wa Sumbawanga umekuwa ni jambo ambalo limekuwa likizungumziwa kwenye vikao mbalimbali vya Baraza la Madiwani wa Manispaa ya Sumbawanga na hata vikao vya Kamati ya Ushauri ya mkoa (RCC) ambapo siku zote

Kaimu Meneja wa TANROADS mkoa wa Rukwa Eng. Jofrey August amesema ujenzi wa uwanja huo kwa kiwango cha lami utahusisha njia ya kuruka na kutua  ndege na viungio vyake, jengo la abiria, barabara za kuingilia uwanjani, sehemu ya kuegesha ndege na magari, mnara wa kuongozea ndege na hali ya hewa na usimikaji wa taa na mitambo ya kuongozea ndege.

August amesema katika mwaka wa fedha 2020/21 serikali Shilingi Bilioni 2.8 kwaajili ya kuanza kazi hiyo ambapo katika ya hizo Milioni 110 ni fedha za ndani na Bilioni 2.7 ni fedha kutoka Benki ya Uwekezaji ya Ulaya ( European Investment Bank).

Tayari kiasi cha Shilingi Bilioni 3.7 zilikwishalipwa kwa wananchi ambao walitakiwa kuondoka kupisha upanuzi wa uwanja huo.

Matangazo

  • TANGAZO LA CHANJO KWA WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO April 26, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2023 March 11, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2023 March 11, 2023
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KAZI ZA UBORESHAJI WA BARABARA KATIKA MANISPAA YA SUMBAWANGA March 01, 2023
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • TANGAZO: KUNYANG'ANYWA VIWANJA VYA WANANCHI WALIOCHUKUA VIWANJA NA KUSHINDWA KUVILIPIA KWA MUDA MREFU

    June 30, 2025
  • MKURUGENZI PENDO MANGALI AHIMIZA UADILIFU NA UWABIKAJI KWA WAHITIMU RIBM

    June 20, 2025
  • SHIRIKIANENI NA SERIKALI KULETA MAENDELEO RUKWA-RC MAKONGORO

    March 16, 2025
  • MD PENDO MANGALI-MSIWE MADALALI WA VIWANJA, CHAPENI KAZI

    November 28, 2024
  • Angalia zote

Video

MANISPAA YA SUMBAWANGA KUTAFUTA MZABUNI WA KUZOA TAKA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa