• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Masuala ya Lishe
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Uratibu na Mipango
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

Waziri Tizeba aagiza wanaouza mbegu feki wafungiwe maduka yao

Ilibandikwa: November 28th, 2017

Waziri wa Kilimo Mh. Charles Tizeba ameiagiza Taasisi ya Uthibitishaji Rasmi wa Mbegu Tanzania (TOSCI) kufanya ukaguzi wa duka kwa duka kwenye maduka ya wafanyabiashara wa pembejeo ili kuwabaini wanaouza mbegu feki na na kuwafungia biashara zao ikibainika wanafanya hivyo.

Amesema kuwa kuwa suala la mbegu feki linawakatisha tamaa wakulima ambao wanategemea kilimo kwaajili ya kuendesha maisha yao na kuwa serikali ya awamu ya tano haitalivumilia jambo hilo na itaendelea kumtetea mkulima nae afaidike kwa kazi anayoifanya.

“Mkulima badala ya kupata gunia 15 hadi 20 anaambulia gunia tano na wananchi wengi hawana uwezo wa kugundua kwamba kinachomsababisha asivune ni mbegu feki, yeye atadhani labda ni hali ya hewa kumbe ni mwizi mmoja kwa tamaa zake amekwamisha maendeleo ya mkulima huyu,” Mh. Tizeba alisisitiza.

Ameyasema hayo alipotembelea shamba la msipazi lililopo katika Kijiji cha china, Wilayani Nkasi na kulalamikiwa na mmiliki wa shamba hilo Salum Sumry aliyeuziwa mbegu feki na Johanes Sanga mwenye duka linaloitwa Gadu Store na kumfungulia kesi mahakamani, kesi ambayo inaendelea hadi leo.

Mh. Tizeba amesema kuwa kesi hizo hazifai kuendeshwa na mkulima badala yake watu wa TOSCI wanatakiwa kuingilia kati ili kupambana na wauzaji hao wa mbegu feki ili kulimaliza tatizo hilo.

Aidha, Waziri Tizeba ameagiza watu wa udhibiti wa mbolea kushughulikia suala la bei elekezi katika mbolea kuhakikisha maduka yote ya pembejeo nchini wanabandika mabango ya bei elekezi za mbolea nje ya maduka yao ili kila mkulima na mnunuzi aweze kuelewa bei hizo na kuongeza kuwa bei hizo elekezi ni kwaajili ya mnunuzi wa mwisho kijijini na sio makao makuu ya Mkoa au Wilaya.

“Huu mzaha wa bei elekezi kuuzwa kwa jumla Mkoani au Wilayani likome, wafuatilie watu waweke matangazo kwenye maduka yao, kwamba bei za Mkoani na Wilayani sio zile zilizotangazwa za mkulima, hizo za mkulima ni kijijini ndipo ananunua ile bei iliyotangazwa na serikali, sio Namanyere kule anatakiwa kuuza chini yah apo,” Mh. Tizeba alifafanua.

Kwa upande wake kaimu Mkurugenzi Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) Lazaro Kitandu amefafanua kuwa mfumo ulioanzishwa na serikali wa ununuzi wa mbolea kwa pamoja unarahisisha upatikanaji wa mbolea nyingi kwa wakati mmoja na hivyo mbolea kuwa na bei ya chini.

“Mfumo huu unadhibiti ununuzi wa mbolea kutoka kwenye chanzo usafirishaji wake, gharama za bandari, gaharama za usafirishaji ndani ya nchi na ile faida anayotaka kuweka mfanyabiashara, kwahiyo hakuna tena nafasi kwa mfanyabiashara kujiongezea bei pasipokjuwa na uhalali, hakuna tena kumnyonya mkulima pasipo halali,” Kitandu alifafanua.

Matangazo

  • TANGAZO LA CHANJO KWA WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO April 26, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2023 March 11, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2023 March 11, 2023
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KAZI ZA UBORESHAJI WA BARABARA KATIKA MANISPAA YA SUMBAWANGA March 01, 2023
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • SHIRIKIANENI NA SERIKALI KULETA MAENDELEO RUKWA-RC MAKONGORO

    March 16, 2025
  • MD PENDO MANGALI-MSIWE MADALALI WA VIWANJA, CHAPENI KAZI

    November 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MANISPAA SUMBAWANGA

    October 01, 2024
  • EDWINE MISASI NAIBU MEYA MPYA MANISPAA YA SUMBAWANGA

    August 27, 2024
  • Angalia zote

Video

MANISPAA YA SUMBAWANGA KUTAFUTA MZABUNI WA KUZOA TAKA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa