• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Masuala ya Lishe
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Uratibu na Mipango
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

SHULE YA WASIOONA MALANGALI YAHITAJI MSAADA ZAIDI KUBORESHA MIUNDOMBINU

Ilibandikwa: July 27th, 2023

Uongozi wa Shule ya Wasiona ya Malangali Manispaa ya Sumbawanga umeiomba serikali kuongeza bajeti ya shule hiyo ili kuweza kukabiliana na changamoto  mbalimbali ikiwa ni pamoja bajeti ndogo ya chakula kwa wanafunzi.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Orthor Mkaranga alimweleza Mkurugenzi wa Mnispaa hiyo kuwa bajeti inayotolewa haitoshelezi kutokana kupanda kwa gharama vyakula lakini pia wanalazimika kuchukua kiasi cha fedha kwaajili ya kuwalipa Wapishi wanne wa shule hiyo.

Mkaranga alisema shule hiyo pia inachangamoto ya kukosa wa usalama wa kutosha kwa wanafunzi na mali za shule hiyo kutokana uzio uliopo kutokamilika, licha kuishukuru serikali kujenga uzio huo ambao kilikuwa ni kilio chao cha muda mrefu.

Shule hiyo ambayo ina wanafunzi wasiona na walemavu wa ngozi pia inakabiliwa na uhaba wa Walimu, sanjari na kukosekana kwa choo kwenye bweni la wanafunzi na kukosekana kwa ulinzi nyakati za mchana, huku akilisemea pia tatizo la uchakavu wa miundombinu ya shule hiyo, jambo lililoungwa mkono na Diwani wa Kata ya Malangali Mary Kipalasha.

Akikabidhi mashine maalumu za kusomea 24 za Orbit 20 zenye thamani ya zaidi ya Shilingi Milioni 46 kwa shule hiyo Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga Catherine Mashalla alisema serikali imekuwa ikijitahidi kutoa elimu bure kwa wanafunzi wa shule za Msingi na Sekondari hivyo hata changamoto zilizopo kwenye shule hiyo zitaendelea kutatuliwa kwa awamu.

Mkurugenzi huyo wa Manispaa aliwataka Wataalamu wa elimu na Walimu wa shule hiyo kuendelea kuboresha mazingira ya shule hiyo kila fedha inapopatikana pasipo kusahau maeneo ya viwanja vya michezo ambavyo vitawafanya Wanafunzi hao kuburudika na kufurahia masomo.

Aidha aliwashukuru Wahisani na wananchi mbalimbali ambao wamekuwa wakitoa misaada kwa shule hiyo na kuendelea kuwaomba kufanya hivyo kwa kushirikiana na serikali.

Shule ya Wasioona ya Malangali ina jumla ya wanafunzi 92 ambapo 47 kati yao ni wasichana.

Matangazo

  • TANGAZO LA CHANJO KWA WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO April 26, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2023 March 11, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2023 March 11, 2023
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KAZI ZA UBORESHAJI WA BARABARA KATIKA MANISPAA YA SUMBAWANGA March 01, 2023
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • SHIRIKIANENI NA SERIKALI KULETA MAENDELEO RUKWA-RC MAKONGORO

    March 16, 2025
  • MD PENDO MANGALI-MSIWE MADALALI WA VIWANJA, CHAPENI KAZI

    November 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MANISPAA SUMBAWANGA

    October 01, 2024
  • EDWINE MISASI NAIBU MEYA MPYA MANISPAA YA SUMBAWANGA

    August 27, 2024
  • Angalia zote

Video

MANISPAA YA SUMBAWANGA KUTAFUTA MZABUNI WA KUZOA TAKA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa