• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Masuala ya Lishe
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Uratibu na Mipango
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

POLISI RUKWA YASHIKILIA WATU 42 KWA TUHUMA MBALIMBALI WAKIWAMO WALIONUNUA RISASI

Ilibandikwa: September 11th, 2021

Anaandika Sammy Kisika.

Jeshi la Polisi mkoani Rukwa linawashikiliwa watu 42 kwa tuhuma mbalimbali, watatu kati yao  wakituhumiwa kununua sanduku la risasi Elfu moja na Mianne zilizookotwa na wavuvi kwenye Ziwa Tanganyika, sanjari na askari watatu wa SUMA JKT ambao wanatuhumiwa kumpiga na kumsababishia kifo mkazi wa mji wa Namanyere wilayani Nkasi.

Katika tukio la kwanza Kamanda wa Polisi mkoani Rukwa William Mwampaghale alisema kuwa watuhumiwa watatu wakazi wa kijiji cha Korongwe huko Nkasi wamekamatwa baada ya kununua sanduku moja lenye risasi ndani yake ambazo ni moja  kati ya masanduku matatu yenye risasi 1493 zilizookotwa na wavuvi kwenye mapango ya yaliyopo kwenye mwambao mwa Ziwa Tanganyika kijijini hapo.

Kamanda Mwampaghale amesema risasi hizo ni za bunduki za kivita aina ya AK47 ambazo bado hazifahamika ni nani alizificha huko, lakini kitendo cha watu hao kujitokeza na kuzinunua risasi hizo kinyume cha sheria kinatia mashaka kuwa malengo yao yalikuwa ni yapi!

Pamoja na watu hao kukamatwa pia Polisi mkoani Rukwa linawashikilia watu wawili wakazi wa mjini Sumbawanga ambao nao wamekatwa wakiwa na risasi 14 za bunduki aina ya AK47 kwenye kitongoji cha Mazwi na Kashai.

Wakati hayo yakitokea Jeshi hilo pia linawashikilia askari watatu wa SUMA JKT ambao ni walinzi wa Chuo cha St.Bakitha cha mjini Namanyere na  raia wengine wawili  wakikabiliwa na tuhuma ya kumpiga hadi kumsababishia kifo mkazi wa eneo hilo wakimtuhumu kwa wizi

Sanjari na hilo pia Polisi mkoani Rukwa wamefanikiwa kumkamata mtuhumiwa anayetajwa kuwa ni mtuhumiwa sugu wa uvunjaji majumbani anayedaiwa kumwibia raia wa kigeni mwenye asili ya Kiamerika Kompyuta mpakato mbili sanjari na vifaa vingine vya kupikia chai aliponaswa navyo kwenye eneo la Kamwanda huko Kirando wilayani Nkasi.

 Polisi mkoani Rukwa pia wamebaini kuibuka kwa wimbi la wizi wa pikipiki ambapo wezi hao wamekuwa na tabia ya kuzibadilisha injini na hata chesesi zake ili mradi tu kumchanganya mmiliki wake , ambapo katika msako wa mwezi mzima jumla ya watu 31 na pikipiki 21 wanashikiliwa kwa tuhuma ya vitendo hivyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA CHANJO KWA WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO April 26, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2023 March 11, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2023 March 11, 2023
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KAZI ZA UBORESHAJI WA BARABARA KATIKA MANISPAA YA SUMBAWANGA March 01, 2023
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • SHIRIKIANENI NA SERIKALI KULETA MAENDELEO RUKWA-RC MAKONGORO

    March 16, 2025
  • MD PENDO MANGALI-MSIWE MADALALI WA VIWANJA, CHAPENI KAZI

    November 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MANISPAA SUMBAWANGA

    October 01, 2024
  • EDWINE MISASI NAIBU MEYA MPYA MANISPAA YA SUMBAWANGA

    August 27, 2024
  • Angalia zote

Video

MANISPAA YA SUMBAWANGA KUTAFUTA MZABUNI WA KUZOA TAKA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa