• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Masuala ya Lishe
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Uratibu na Mipango
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasimali watu
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Manunuzi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
        • Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka Ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Utunzaji wa Mazingira
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

MADIWANI WANAWAKE JENGENI UJASIRI WA KUTETEA BAJETI KWA HUDUMA ZA KIAFYA, ELIMU NA MAJI-

Ilibandikwa: December 13th, 2021

Ameandika Sammy Kisika.

Madiwani wanawake katika mikoa ya Rukwa na Katavi wametakiwa kushiriki kikamilifu kwenye upangaji wa bajeti za halmashauri zao huku wakiweka umakini katika utetezi wa makundi maalumu kwenye jamii zao.

Chachu ya Madiwani hao inatokana na mafunzo waliyoyapata ambayo yanaratibiwa na Mtandao wa Kijinsia TGNP ambapo imewakutanisha na kuwapa elimu juu ya njia bora ya kujadili bajeti katika mikoa hiyo.

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti ambaye alikuwa Mgeni rasmi katika ufunguzi wa mafunzo hayo aliwaambia Madiwani hao kuwa muda umefika wao kuonesha michango yao katika Mabaraza yao ya Madiwani badala ya kukaa kimya.

Mkirikiti alisema ipo haja ya Madiwani hao kuendelea kujengewa uwezo ili waweze kuhoji bajeti zinazopangwa kwenye miradi au huduma muhimu za afya, maji na elimu.

“Fedha nyingi zimekuwa zikitolewa kwenye miradi hiyo lakini hakuna anayehoji kuwa hapa kuna fedha hii ililetwa kwenye miradi ya afya au elimu, fungukeni sasa kwani huo ni muda wa kuitetea jamii ili huduma bora ziweze kupatikana”.alisema Mkirikiti

Alisema mchango wao katika jamii ni mkubwa hususan kipindi hiki ambapo Rais Samia Suluhu anaongoza, hivyo nao wanatakiwa kumuunga mkono kwa vitendo na kusimamia miradi inayofanyika kwenye maeneo yao.

Aidha Mkirikiti aliwapongeza TGNP kwa kuendesha mafunzo hayo ambayo anaamini kuwa maarifa wanayopata Madiwani hao yataleta mabadiliko kwa kuhoji mambo mengi yanayojadiliwa kwenye Mabaraza yao.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mtandao wa Madiwani hao ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Lwiche katika Manispaa ya Sumbawanga Adolphina Konongo alisema anaamini kuwa hivi sasa wanauelewa wa kutosha kuhusu masuala ya bajeti tofauti na siku za nyuma ambapo walikuwa wakishiriki mabaraza yao na kukaa kimya muda mwingi.

“Nguvu yetu kubwa lazima tuielekeze kwenye miradi ya afya ambako zahanati zinajengwa na hakuna dawa, huku akinamama wakitembea umbali mrefu kufuata huduma hizo, hii sasa ifike mwisho maana tunapoteza wanawake na wazee wengi”.alisema Konongo.

Mratibu wa mafunzo hayo kutoka TGNP Clara Mcharo licha ya kufurahishwa na uelewa  wa  Madiwani hao aliwataka kujenga dhamira ya kweli katika kutetea masuala ya kiafya na huduma bora za kielimu kwa watoto kwenye maeneo yao.

“Utakuwa mzazi anakwenda jifungua zahanati anaambiwa aende na ndoo ili apewe kondo lake baada ya kujifungua, eti kwasababu zahanati au kituo cha afya hakina sehemu ya kuchomea uchafu, hii sio sawa, twendene tukapambane kwenye bajeti hayo mambo hayo yaishe”.alisema Clara.

Mtandao wa kijinsia wa TGNP licha kuwafundisha Madiwani hao namna ya kushiriki kwenye upangaji wa bajeti lakini wamefundishwa namna bora ya uongozi kwenye nafasi zao.

Matangazo

  • TANGAZO LA CHANJO KWA WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO April 26, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2023 March 11, 2023
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2023 March 11, 2023
  • TANGAZO LA ZABUNI YA KAZI ZA UBORESHAJI WA BARABARA KATIKA MANISPAA YA SUMBAWANGA March 01, 2023
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • SHIRIKIANENI NA SERIKALI KULETA MAENDELEO RUKWA-RC MAKONGORO

    March 16, 2025
  • MD PENDO MANGALI-MSIWE MADALALI WA VIWANJA, CHAPENI KAZI

    November 28, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MANISPAA SUMBAWANGA

    October 01, 2024
  • EDWINE MISASI NAIBU MEYA MPYA MANISPAA YA SUMBAWANGA

    August 27, 2024
  • Angalia zote

Video

MANISPAA YA SUMBAWANGA KUTAFUTA MZABUNI WA KUZOA TAKA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa