• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL
SUMBAWANGA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Manispaa
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi & Mipango Miji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mazingira na Taka Ngumu
      • Mipango na Uchumi
      • Utawala & Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Internal Audit Unit
      • Legal Service Unit
      • Info,Comm & Techno Unity
      • Procurement Management Unity
  • Fursa za uwekezaji
    • Natural Resource and Environmental Consarvertion
  • Huduma
    • Afya
    • Education
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati na majukumu yake
      • Fedha na Utawala
      • Uchumi, Elimu & Afya
      • Mipango miji & Mazingira
    • Ratiba za Vikao
      • For Councilors
      • For Hon. Mayor
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
    • Huduma za Kisheria
    • Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Makala
    • Michezo & Burudani

MADIWANI WANAWAKE JENGENI UJASIRI WA KUTETEA BAJETI KWA HUDUMA ZA KIAFYA, ELIMU NA MAJI-

Ilibandikwa: December 13th, 2021

Ameandika Sammy Kisika.

Madiwani wanawake katika mikoa ya Rukwa na Katavi wametakiwa kushiriki kikamilifu kwenye upangaji wa bajeti za halmashauri zao huku wakiweka umakini katika utetezi wa makundi maalumu kwenye jamii zao.

Chachu ya Madiwani hao inatokana na mafunzo waliyoyapata ambayo yanaratibiwa na Mtandao wa Kijinsia TGNP ambapo imewakutanisha na kuwapa elimu juu ya njia bora ya kujadili bajeti katika mikoa hiyo.

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti ambaye alikuwa Mgeni rasmi katika ufunguzi wa mafunzo hayo aliwaambia Madiwani hao kuwa muda umefika wao kuonesha michango yao katika Mabaraza yao ya Madiwani badala ya kukaa kimya.

Mkirikiti alisema ipo haja ya Madiwani hao kuendelea kujengewa uwezo ili waweze kuhoji bajeti zinazopangwa kwenye miradi au huduma muhimu za afya, maji na elimu.

“Fedha nyingi zimekuwa zikitolewa kwenye miradi hiyo lakini hakuna anayehoji kuwa hapa kuna fedha hii ililetwa kwenye miradi ya afya au elimu, fungukeni sasa kwani huo ni muda wa kuitetea jamii ili huduma bora ziweze kupatikana”.alisema Mkirikiti

Alisema mchango wao katika jamii ni mkubwa hususan kipindi hiki ambapo Rais Samia Suluhu anaongoza, hivyo nao wanatakiwa kumuunga mkono kwa vitendo na kusimamia miradi inayofanyika kwenye maeneo yao.

Aidha Mkirikiti aliwapongeza TGNP kwa kuendesha mafunzo hayo ambayo anaamini kuwa maarifa wanayopata Madiwani hao yataleta mabadiliko kwa kuhoji mambo mengi yanayojadiliwa kwenye Mabaraza yao.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mtandao wa Madiwani hao ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Lwiche katika Manispaa ya Sumbawanga Adolphina Konongo alisema anaamini kuwa hivi sasa wanauelewa wa kutosha kuhusu masuala ya bajeti tofauti na siku za nyuma ambapo walikuwa wakishiriki mabaraza yao na kukaa kimya muda mwingi.

“Nguvu yetu kubwa lazima tuielekeze kwenye miradi ya afya ambako zahanati zinajengwa na hakuna dawa, huku akinamama wakitembea umbali mrefu kufuata huduma hizo, hii sasa ifike mwisho maana tunapoteza wanawake na wazee wengi”.alisema Konongo.

Mratibu wa mafunzo hayo kutoka TGNP Clara Mcharo licha ya kufurahishwa na uelewa  wa  Madiwani hao aliwataka kujenga dhamira ya kweli katika kutetea masuala ya kiafya na huduma bora za kielimu kwa watoto kwenye maeneo yao.

“Utakuwa mzazi anakwenda jifungua zahanati anaambiwa aende na ndoo ili apewe kondo lake baada ya kujifungua, eti kwasababu zahanati au kituo cha afya hakina sehemu ya kuchomea uchafu, hii sio sawa, twendene tukapambane kwenye bajeti hayo mambo hayo yaishe”.alisema Clara.

Mtandao wa kijinsia wa TGNP licha kuwafundisha Madiwani hao namna ya kushiriki kwenye upangaji wa bajeti lakini wamefundishwa namna bora ya uongozi kwenye nafasi zao.

Matangazo

  • Waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2021 December 18, 2020
  • Walichaguliwa Kidato cha Kwanza 2021 -PDF December 18, 2020
  • KALENDA YA UTEKELEZAJI WA MITAALA YA ELIMU YA AWALI NA MSINGI TANZANIA BARA,JANUARY 2022. February 15, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 HALMASHAURI YA MANISPAA SUMBAWANGA. December 07, 2019
  • Angalia zote

Habari za Karibuni

  • RC QUEEN SENDIGA AANZA NA KUPAMBANA NA SUALA LA UDUMAVU RUKWA

    August 07, 2022
  • IDARA YA KILIMO MANISPAA YA SUMBAWANGA YASHAURIWA KULIMA KWA WINGI BROKOLI

    August 05, 2022
  • MAZIWA YA SUMBAWANGA MILK YANAPENDWA NA WATU WENGI NANENANE

    August 03, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KWENYE SENSA H/MANISPAA YA SUMBAWANGA

    July 27, 2022
  • Angalia zote

Video

MANISPAA YA SUMBAWANGA KUTAFUTA MZABUNI WA KUZOA TAKA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • History
  • Councilors
  • Photo Gallery

Viunganishi vinavyofanana

  • Public Servant portal
  • Download your Salaryslip here
  • Looking for a job in Public Sector?
  • Get everything from the government
  • Rukwa
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Sumbawanga Municipal Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga

    Simu ya Mezani: +255252802163

    Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255

    Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Uhuru binafsi
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa