Kitengo cha Mawasiliano
Wakurugenzi wa Halmashauri mkoani Rukwa wametakiwa kuyapa fursa Mabaraza ya Wafanyakazi kwenye halmashauri zao kuweza kujadiliana changamoto zinazowakabili ili waweze kuzitatua changamoto zao sehemu za kazi kwa lengo la kuongeza uwajibikaji na tija katika utumishi.
Rai hiyo imetolewa na Kaimu Katibu Tawala wa mkoa wa Rukwa Donald Nssoko wakati uzinduzi wa Baraza la Wafanyakazi la Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga ambapo Watumishi hao walipata fursa ya kueleza na kupewa ufafanuzi wa changamoto mbalimbali zinazowakabili.
Nssoko alisema kuwa utendaji kazi wa Mabaraza ya Wafanyakazi kwenye halmashauri ni sawa ni kioo ambacho Wakurugenzi wanaweza kukitumia kuona taswira ya ufanisi wa halmashauri zao na kutumia nafasi hiyo kurekebisha dosari zilizopo ili kazi ziweze kufanyika huku Watumishi waweze kufanyakazi kwa kujituma na ari pia.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa Sumbawanga Kulanga Kayanga alisema maelekezo yaliyotolewa na serikali ya mkoa yamepokelewa na kila Mtumishi hivyo kilichobaki ni suala uwajibikaji katika maeneo ya kazi kwa kila mtu kutimiza wajibu wake ili kupata haki za kiutumishi lakini pia kuwatumikia wananchi.
Katibu Msaidizi wa Baraza la Wafanyakazi la Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga Edina Mbise ambaye ni mmoja kati ya viongozi walichaguliwa kwenye kikao hicho alisema wamechukua kijiti cha uongozi wakiwa na mikakati ya kusikiliza changamoto za Watumishi na kuziwasilisha kwa Mwajiri ili ziweze kutatua kwa kufuata ngazi husika.
Saada Kimanta aliyehudhuria kikao hicho akiwa ni Mtendaji wa kata ya Mzwi alisema awali walikuwa na changamoto nyingi zikiwapo za malimbikizo ya mishahara na malipo fedha za likizo lakini kupitia kikao hicho Kaimu Mkurugenzi Kayanga amezitolea ufafanuzi na ahadi ya kuzishughulikia, hivyo wana imani kuwa matatizo yao yatakwisha baada ya kuwasilishwa serikalini.
Sumbawanga Municipal Council
Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga
Simu ya Mezani: +255252802163
Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255
Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz
HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa