Kwa mujibu wa sensa ya Mifugo ya mwaka 2016/2017, Manispaa ina Jumla ya Ng’ombe 36,417, Mbuzi 19,270 Kondoo 1,085, Punda 1058 ,Nguruwe 13,010 ,Mbwa 8,699, Kuku 104,378 , Bata ni 7,938. Hali ya miundombinu katika mifugo ni kama inavyojionesha katika jedwali lifuatalo:-
Hali ya miundombinu ya Mifugo katika Halmashauri
NA |
AINA YA MIUNDOMBINU |
HITAJI |
YALIYOPO |
UPUNGUFU |
1
|
Majosho
|
14 |
12 |
2 |
2
|
Mnada
|
1 |
1 |
0 |
3
|
Machinjio
|
1 |
2 |
1 |
4
|
Makaro ya kuchinjia
|
24 |
5 |
19 |
5
|
Mabanda ya ngozi makubwa
|
24 |
5 |
19 |
6
|
Vibanio vya kudumu
|
24 |
4 |
20 |
7
|
Marambo
|
0 |
0 |
0 |
8
|
Vituo vya maendeleo ya Mifugo
|
7 |
1 |
6 |
Ili kuhakikisha mifugo inakuwa na afya na Salama kwa walaji, Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga imeanza kutoa chanjo mbali mbali kwa mifugo kwa kipindi cha 2017/2018 kama inavyoonekana kwenye jedwali hapo chini. Mpaka sasa mbwa 2,131 wamechanjwa kati ya mbwa 8,699 sawa na asilimia 27.23 na huduma ya chanjo bado inaendelea.
Malengo ya kutoa chanjo ya mifugo Mwaka 2017/2018
NA |
AINA MIFUGO |
AINA YA CHANJO |
LENGO |
WALIOCHANJWA |
|
1
|
Mbwa
|
Kichaa cha Mbwa
|
8,699
|
2,392
|
27.50%
|
2
|
Kuku wa asili
|
Mdondo
(Newcastle disease) |
84,180
|
17,916
|
21.28
|
3
|
Kuku
|
Mdondo
(Newcastle disease) |
20,198
|
28,040
|
50.12
|
Zoezi la upigaji chapa ng’ombe katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga lilianza tarehe 10/8/2017, ambapo hadi sasa jumla ya ng’ombe 32,964 wamepigwa chapa dhidi ya ng’ombe 36,417 waliokisiwa sawa na asilimia 91% ya ng’ombe wote wa Manispaa ya Sumbawanga.
Sumbawanga Municipal Council
Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga
Simu ya Mezani: +255252802163
Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255
Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz
HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa