MAJUKUMU YA KITENGO CHA SHERIA
1. Kufuatilia ,Kusimamia na kutetea kesi za Halmashauri ya Manispaa zilizoko Mahakamani baada ya siku 1 tu kuwepo kwa kesi hizo Mahakamani na kuzingatia taratibu za uendeshaji wa kesi Mahakamani .
2. Kuandaa na kusajili nyaraka za kimahakama zinazohusiana na kesi zilizoko Mahakamani baada ya siku 21 baada ya kupokea hati za madai .
3. Kusimamia sheria mama na sheria ndogo za halmashauri kwa kuchukua hatua za kisheria kwa wanaokiuka sheria ndani ya mamlaka ya Halmashauri ikiwa ni pamoja na kuwafikisha polisi na Mahakamani baada ya kuwapatia notisi ya siku 30 za kutii sheria zilizopo na kuonekana wanakaidi.
4. Kuandaa rasimu ya sheria Ndogo na au kufanya marekebisho ya sheria Ndogo zilizopitwa na wakati ndani ya siku 7 baada ya kupata mapendekezo kutoka kwenye menejimenti (CMT).
5. Kutoa elimu au taarifa kwa umma kuhusu sheria Ndogo za Halmashauri zinazokusudiwa kutungwa siku 14 kabla ya halmashauri kupitisha sheria hizo.
Sumbawanga Municipal Council
Anuani ya Posta: P.O.BOX 187, Sumbawanga
Simu ya Mezani: +255252802163
Simu ya Kiganjani: +255 735519681/ +255
Barua pepe: md@sumbawangamc.go.tz
HakiMiliki ©2017 Sumbawangamc . Haki Zote Zimehifadhiwa